Habari Kali
Loading...

ANTI LULU: Natamani kumzalia DIAMOND, Sijali hata kama WEMA ataniloga!!

Mbinu Za Kumfikisha Kileleni Mwanamke Mwenye Makalio Makubwa Kwa Haraka, Bonyeza Hapa chini== >
MOYO unahifadhi mengi! Msichana wa mjini asiyeishiwa matukio Bongo, Lulu Mathias Semagongo ‘Anti Lulu’ amefunguka kwamba yupo tayari kuzaa na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kwani amepata taarifa kwamba anasaka mtoto lakini wanawake anaokuwa nao hawataki kumzalia, Ijumaa Wikienda linakupasha.

BILA KUMUNG’UNYA MANENO

Akizungumza na gazeti hili bora la mastaa Bongo akiwa dukani kwake Kinondoni jijini Dar, wikiendi iliyopita, Anti Lulu bila kumung’unya maneno, alifunguka kwamba hivi karibuni alifuatwa na ndugu wa karibu wa Diamond au Dangote kama anavyopenda kujiita na kumuomba afanye jitihada azae naye.

MAKUBWA!

Alidai aliambiwa kuwa kila Diamond akimpa kibendi mwanamke, huwa mwanamke huyo anakwenda kukitoa bila hata ridhaa yake (Diamond).
“Ndugu wa Diamond alinifuata hapa dukani kwangu akanitaka nizae na Dangote kwani anasaka sana mtoto na kila akimpa mwanamke mimba huwa anaichoropoa bila kuafikiana naye.“Sababu kubwa ya wanawake hao kutoa mimba ni kutokana na mpenzi wa Diamond ambaye ni Wema (Isaac Sepetu) kudaiwa kuloga ili mwanamke yeyote asizae naye na kila akimpa mimba mwanamke inatoka au anakwenda kutoa mwenyewe bila sababu yoyote,” alisema Anti Lulu.

Msanii wa filamu za Kibongo Lulu Mathias.
Msanii wa filamu za Kibongo Lulu Mathias.
Pamoja na tetesi hizo, Anti Lulu alisema haogopi lolote kwani amejizatiti ndiyo maana amejitokeza hadharani na kutaka kuzaa na Diamond.

IMANI

Anti Lulu alisema kwamba anaamini Diamond atamkubali japokuwa hawajawahi kuzungumzia hiyo ishu wakiwa pamoja na kwamba walishakutana na kuzungumza mambo mengine.
“Nataka na nimejizatiti vilivyo kwa ajili ya kumzalia Diamond ‘kabebi’ kazuriii…
“Nataka nione hiyo kulogwa inakuwaje hao wanaotoaga mimba zake bila sababu?
MTOTO MZURI
“Naamini mimi nitamzalia mtoto mzuri kabisa kwani nimejipanga tayari na siogopi kitu chochote.
“Diamond hajawahi kunitongoza ila kuna siku moja tulionana maeneo ya Kinondoni halafu nikaja kuambiwa na mmoja wa marafiki zake kwamba aliponiona siku hiyo alinisifia.
“Niliambiwa alisema kwamba mimi ni mwanamke mzuri na umbo langu ni zuri hivyo naomba akubali tu nimzalie jamani,” alisema Anti Lulu ambaye aliwahi kuwa prizenta wa runinga na mwigizaji wa sinema za Kibongo.

BIFU?

Anti Lulu alidai kwamba japokuwa anaamini kabisa kwamba Wema atakasirika, hatajali kama mbwai iwe mbwai na yupo tayari kuanzisha naye bifu zito.
Staa Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa kwenye pozi lenye utata.
Staa Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa kwenye pozi lenye utata.
Alisema kila mmoja atakuwa na nafasi yake kwa Diamond na kwamba kikubwa anataka kuzaa na Diamond halafu amkabidhi mtoto kila mmoja aendelee na maisha yake.

NENO!

“Najua Wema atakuwa na bifu na mimi lakini sijali kwa sababu nimeamua na yeye ni mpenzi wa Diamond tu siyo mke wake kwani hawajafunga ndoa.
“Angekuwa ni mkewe ndiyo ningeogopa lakini hivihivi sihofii chochote,” alisema Anti Lulu.

DIAMOND, WEMA NA PENNY

Diamond aliwahi kuripotiwa kumpa ujauzito aliyekuwa mpenzi wake, Penniel Mungilwa ‘Penny’ lakini baada ya muda mfupi ilidaiwa kuchoropoka.Pia aliwahi kudaiwa kumpachika kibendi Wema ambaye naye ilidaiwa ilichoropoka.
Kwa upande wake Anti Lulu aliwahi kutoka na wanaume kadhaa wakiwemo Bond Bin Sinan na Amani ambao hakufanikiwa kuwazalia watoto.

SWALI LENYE HOJA!

Baadhi ya watu waliomsikia Anti Lulu akitangaza ishu hiyo walijiuliza swali moja tu: ‘Hivi kweli Anti Lulu huyuhuyu anaweza kuwa mama bora?’Diamond hakupatikana ili kufikishiwa ujumbe huo na kujua namna alivyopokea taarifa hiyo ya Anti Lulu. 

Hizi ndio sehemu 12 zinazompa Raha mwanamke wakati wa Tendo, Bonyeza Hapa chini== >


Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA VIDEO CHAFU YA AGNESS MASOGANGE== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright ZEE LA UDAKU | Designed By Code Nirvana
Back To Top