Habari Kali
Loading...

FUTARI YAZUA BALAA! APEWA KIPIGO CHA MBWA MWIZI BAADA YA KUIBA KITI


Dustan Shekidele, Morogoro LA haula! Mwanamke aliyefahamika kwa jina moja la Asha, mkazi wa Mtaa wa Area Six, Kata ya Kichangani mkoani  hapa ambaye alikuwa kwenye swaumu ya Mfungo wa Ramadhani, amejikuta akilazimika kutengua swaumu na kumpa kichapo mwanaume aliyeiba futari na kiti chake cha plastiki alichokuwa amekalia nje ya nyumba akipika futari hiyo.
Akihojiwa baada ya kuminyiwa kichapo.
TUKIO KAMILI
Tukio hilo la aina yake, lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo wakati paparazi wetu anawasili kwenye eneo la tukio, alikuta kasheshe bin tafrani ikiendelea. Mbali na mwanamke huyo, wananchi wenye ghadhabu nao walikuwa wakimshikisha adabu mwanaume huyo huku wakidai ni mwizi.

MAELEZO YA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo, awali mwanamke huyo alikuwa nje ya nyumba yake akipika futari huku akiwa amekalia kiti hicho.


Akiomba kuachiwa baada ya kupewa kichapo kikali.
“Ghafla si akapata udhuru uliomlazimu aingie ndani. Akaacha futari ikitokota jikoni. Amefanya yake kule ndani, akakumbuka ameacha futari jikoni, akatoka.“Kufika! Kwanza akaona futari imepungua. Sasa ile anataka kukaa, kiti nacho hakipo. Akashangaa.”
ATAFUTA KITI, AMWONA NACHO MTU
Chanzo kiliendelea kudai kuwa, mwanamke huyo alianza kukisaka kiti chake sehemu mbalimbali nyumbani hapo lakini bila mafanikio. Alipotupa macho mbali na nyumbani, akamwona nacho huyu mwanaume amekibeba akitambaa zake.

“Ndipo mama bila kujali swaumu, akaingia ndani. Akachukua kirungu na sime na kumfukuza mpaka akamkamata na kuanzia kumwangushia kipondo huku jamaa akikitupa kile kiti kichakani kwa lengo la kupoteza ushahidi,” kilisema chanzo hicho.
WANANCHI WAINGILIA KATI
Baadhi ya wananchi wanaoaminika kuwa na hasira kali nao waliamua ‘kununua’ kesi hiyo ambapo na wao walichukua silaha mbalimbali, yakiwemo mawe na kuanza kumbonda mwanaume huyo mpaka damu chapachapa.

Anayedaiwa kuibiwa futari akimpiga kwa hasira.
BODABODA NUSURA WAMTOE UHAI, WAMVUNJA MGUU
Baadhi ya madereva wa bodaboda walipomwona mwanaume huyo anazidi kuchakaa uso kwa kipigo, badala ya kumwokoa, waliingilia kati na kutaka kumchoma moto lakini wasamaria wema walipinga kitendo hicho na kumuokoa kwa kumkimbizia kwenye Kituo cha Polisi cha Nanenane kilicho jirani na eneo la tukio.

Hata hivyo, wakati akikimbizwa polisi, bodaboda hao waliamua kumgonga na pikipiki kwa makusudi na mmoja wao alifanikiwa kumvunja mguu.
MAMA MWENYE FUTARI
Alichonifanyia siyo haki kabisa, kama alikuwa na njaa, angeniambia, ningempakulia futari akala kuliko kuniibia.

ACHAKAZWA SURA NA MKE MWENZIYE


Na Stephano Mango, Ruvuma
“Dunia imeharibika na binadamu hawana upendo wamegeuka kuwa na tabia kama za wanyama kila kukicha…” hiyo ni kauli yake Rehema Gwaya (41) mkazi wa Barabara ya Sokoine, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Rehema Gwaya akiwa na majeraha usoni baada ya kumwagiwa mafuta ya moto.
Rehema ambaye ni mjasiriamali mdogo anayejishughulisha na kuuza juisi, alipatwa na mkasa wa kumwagiwa mafuta ya moto ya kupikia ambayo yalikuwa yanatumika kwa ajili ya kuchomea maandazi.
Inadaiwa aliyefanya unyama huo ni mke wa  shemeji yake baada ya kutokea sintofahamu ya usafi wa mazingira ya nyumbani kwao, kama anavyojieleza:
“Tukio limetokea mwishoni mwa Mei nikalazwa mwanzoni mwa Juni hadi sasa Julai ambapo Daima Said (13) ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Msingi Luseti ninayeishi naye aligombana na mke wa shemeji yangu, Zefania Chimgege, chanzo kikiwa ni suala la usafi wa mazingira kwani mama huyo alipaswa kwenda kusafisha choo akakataa kukawa na mzozo mkubwa.
“Mzozo huo ulitokea mimi nikiwa sipo, nilikuwa kwenye biashara zangu, niliporudi nyumbani nilimfuata mama Chimgege ili anipe maelezo, ghafla akanivamia na kuanza kunishambulia kwa maneno makali yaliyoambatana na matusi.

Akimnyonyesha mwanaye.
“Wakati huo mume wake alikuwa anachoma maandazi kwa ajili ya biashara yake, wakati naendelea kutafakari kauli chafu alizozitoa dhidi yangu, nilishitukia nikimwagiwa mafuta ya moto usoni, papo hapo nilianguka chini jambo  lililompa nafasi mama huyo kunikalia na kuanza kunichuna ngozi iliyobabuka.
“Nilipoteza fahamu na kujikuta nipo Hospitali ya Mkoa Songea, nimelazwa wodi ya wanawake nikiwa na majeruhi usoni na kwenye matiti, hivyo naendelea kupata matibabu.
“Nawaomba Watanzania wenye mapenzi mema kunisaidia kwani kwa sasa siwezi kufanya shughuli yoyote kutokana na kuuguza majeraha ya moto ambayo yana maumivu makali na hapa nilipo nina mtoto mdogo wa miezi tisa ambaye ananyonya.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Serikali ya Mkoa Songea, Dk. Benedikto Ngaiza amethibitisha kumpokea mgonjwa huyo ambapo alisema anaendelea kupatiwa matibabu.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma,  ACP Mihayo Mikhela amekiri kutokea kwa tukio hilo na amethibitisha kuwa mtuhumiwa anashikiliwa wakati upelelezi unaendelea.

MAHABUSU ADAIWA KUFIA KITUO CHA POLISI!


Na Shani Ramadhani MSIBA! Mwanaume aliyefahamika kwa jina la Juma Abdallah Juma (51), mkazi wa Bunju ‘B’ jijini  Dar anadaiwa kufia kwenye Kituo cha Polisi Oysterbay, Dar huku ndugu wakiibuka na madai kuwa, alipigwa na polisi wa kituo alichowekwa mahabusu, Uwazi lilifuatilia.
Marehemu Juma Abdallah Juma enzi za uhai wake.
Akizungumza na gazeti hili, dada wa marehemu Juma, Mwanaidi Abdallah alisema, awali, marehemu na ndugu zake wawili, Muhisan (42) na Baraka (30) walikamatwa Juni 16, mwaka huu na askari wa vituo vya polisi vya Wazo, Boko na Tegeta kwa madai wanahusika na wizi wa magari matatu.
Ndugu huyo alisema, askari hao waliyataja magari hayo kuwa ni Toyota Prado (thamani ya Sh. milioni 30), Mistubishi (Sh. milioni 30) na BMW (Sh. milioni 65). 
Iliendelea kudaiwa kuwa, askari hao waliwachukua na kuwapeleka vituo tofauti ambapo, Muhisan alipelekwa  Kituo cha Tegeta, marehemu Juma, Wazo na Baraka alisukumizwa Boko.
“Baada ya kusikia hivyo, tulikwenda Tegeta, tulimkuta Muhisan, akatuambia Juma yupo Kituo cha Polisi Wazo lakini hali yake si nzuri (hakufafanua kivipi). Lakini baadaye wote walihamishiwa Kituo cha Kawe. Tulipofika huko pia tukazuiwa kumuona, polisi wakasema ndugu yetu ni jambazi.
“Tulihangaika sana. Baada ya wiki moja tukamuona tena kwa kuomba kwa Mkuu wa Upelelezi wa Wazo. Kusema kweli hali yake ilikuwa inasikitisha. Alikuja kutusalimia akiwa anatambaa, amevimba uso, mikono, miguu yote na mmoja ulikuwa umepasuka.
“Tuliomba apelekwe hospitali  kufanyiwa uchunguzi tujue anasumbuliwa na nini, tukaambiwa tutoe shilingi 15,000  nauli ya Bajaj.
“Siku ya pili tulipokwenda tukakuta amefungwa bandeji kwenye miguu, wakasema tumnunulie dawa ya kupunguza maumivu, tukafanya hivyo.“Mke wa Muhisan alidamka kupeleka chai kwa mumewe, kufika akaambiwa ndugu zenu wote leo wamepelekwa Mahakama ya Kinondoni.
“Tulipopata taarifa hizo... tulijipanga na wadhamini tukaenda mahakamani. Kufika tukakuta ndiyo wameitwa na wakati huo Juma amebebwa na Muhisan na Baraka hawezi kutembea sawasawa. Walisomewa mashitaka  yao kuwa waliiba magari kwenye Yadi ya Mazrui iliyopo Kijitonyama (Dar) wakiwa wametumia silaha aina ya bastola.
“Washitakiwa wakaandikiwa kwenda Gereza la Segerea lakini wakaambiwa gari limejaa, ikabidi wapelekwe Kituo cha Polisi Oysterbay kukaa kwa muda.
“Jumanne ya wiki iliyopita, tukapeleka chakula asubuhi, Juma hakuweza kula. Tulipokwenda baadaye, Muhisan akasema hali ya Juma ni mbaya. Tukafanya mpango wa  gari la magereza akatibiwe lakini kabla gari halijafika, polisi walikwenda kumchukua kwa kumbeba kwenye machela, wakamuweka kwenye gari, kabla hawajaondoka, Juma alikata roho.
“Sisi tulitoka pale kwenda Hospitali ya Mwananyamala na wao walielekea huko. Walipofika wakaufikisha mwili moja kwa moja mochwari,” alisema Mwanaidi kwa huzuni.
Ili kujua ukweli wa mambo yota hayo, Uwazi lilimtafuta Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camillius Wambura ambaye alikiri kuwa na taarifa za kifo cha Juma, lakini akasema:
“Juma aliletwa hapa baada ya kukosa nafasi kwenye  gari alilokuwa anatakiwa kupanda kwenda Segerea. Habari za kupigwa au kutokupigwa zitatafsiriwa baada ya uchunguzi kufanyika kwa sababu mpaka sasa mwili wake bado upo mochwari kwa uchunguzi (kesho).
“Mtuhumiwa alifariki dunia baada ya kuugua akiwa kituo cha polisi kabla ya kupelekwa hospitali kupata matibabu ya ugonjwa wake.”

UKATILI WA KUTISHA! MTOTO MIAKA 5 ATEKWA DAR, ABAKWA HADI KUFA


Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa
NIkweli dunia imekwisha! Ni vigumu kuamini mtoto mdogo ambaye anahitaji uangalizi na ulinzi kutoka kwa jamii anageuzwa mwanamke na kuingiliwa kwa nguvu hadi mauti. Huu ni unyama na ukatili wa hali ya juu.

Mtoto Ester Banzi enzi za uhai wake.
Tukio hilo la kutisha lilitokea katikati ya wiki iliyopita, Tabata Msimbazi jijini Dar ambapo mtoto Ester Banzi ,5, (pichani) alikutwa na mauti baada ya kuingiliwa kimwili na mwanaume ambaye inadaiwa alimteka kwanza.
Akizungumza na Gazeti la Uwazi kwenye msiba huo, mama mdogo wa marehemu Ester aliyejitambulisha kwa jina la Watende Hamis huku akitokwa machozi mfululizo, alisema:

“Siku ya tukio, ilikuwa saa 5:30 asubuhi tukiwa nyumbani, dada (mama wa marehemu aitwaye Rebeka) alikuwa ameinjika sufuria ya ugali jikoni kwa ajili ya chakula cha mchana.
“Akamtuma Ester dukani akanunue unga. Alimpa shilingi 1,200. Si mara ya kwanza Ester kutumwa dukani kwa vile ni jirani tu.

“Tulimsubiri Ester arudi na unga lakini alichukua muda mrefu. Ikabidi tumfuate dukani, hatukumuona. Tuliwauliza watoto wenzake ambao anapenda kucheza nao, wakasema walimuona amebeba mfuko cha Rambo huku akiongozana na baba mmoja.

Jeneza lililobeba mwili wa marehemu likiwa tayari kwa ajili ya kuagwa.
“Basi, tuliendelea kumtafuta bila mafanikio. Ikabidi tutoe taarifa kwa baba yake ambaye akaingiwa na wasiwasi, akaenda kutoa taarifa kwenye Kituo cha Polisi Tabata Shule.“Ndani ya masaa matatu baba yake akatupigia simu kwamba mwili wa Ester umeokotwa huku ukionekana alibakwa na kuharibiwa vibaya.”
Naye kijana anayeuza duka ambalo marehemu alitumwa kununua unga, bila kutaja jina lake alikiri Ester kufika dukani hapo na kupimiwa unga kisha akaondoka.
Baadhi ya wananchi majirani na maeneo hayo waliohojiwa na waandishi wetu kuhusiana na tukio hilo walisema kwamba wao walimuona mtoto huyo akifuatana na mwanamume mmoja, lakini hawakumtilia mashaka kutokana kwamba walifikiri ni ndugu yao.
Mtu mmoja ambaye mwili wa marehemu ulikutwa jirani na nyumba yake, naye alizungumzia tukio hilo:
“Sisi tulisikia sauti ya mtoto akiomba msaada. Tulipata hofu ikabidi tukaangalie eneo lile ndipo tulipouona mwili wa mtoto huyo. Tulipomchunguza tukagundua alibakwa kwani nguo yake ya ndani ilikuwa pembeni.

“Inaonekana huyo mtu hakuchukua muda mrefu kufanya kitendo hicho. Tulimpigia simu Mkuu wa Kituo cha Polisi Tabata Shule, Afande Kobelo akaja na timu yake. Hili tukio nahisi lina ushirikina ndani yake.”
Mmoja wa askari aliyefika katika eneo la tukio ambaye hakutaka kutaja jina lake kwa vile siyo msemaji mkuu wa jeshi hilo alisema mwili wa mtoto huyo ulionekana kuingiliwa kimwili, marehemu alivunjwa shingo na kutobolewa upande wa kushoto kichwani.Marehemu Ester alizikwa wiki iliyopita mkoani Morogoro. Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu. Amina.

MAITI YAKOHOA, YAFUMBUA MACHO

1Maajabu ya Bagamoyo! Katika hali ya kushtua, familia yenye makazi yake, Magomeni, Bagamoyo mkoani Pwani, imejikuta kwenye mauzauza baada ya ndugu yao kufariki dunia huku akidaiwa kukohoa, kufumbua macho na kuonesha dalili za kuwa hai, pamoja na kwamba daktari alithibitisha kifo.
WAOMBOLEZAJI WATIMUA
Katika tukio hilo lililosababisha waombolezaji kutimua mbio lililojiri Juni 28, mwaka huu, binti wa familia hiyo, Tunu Shabani (36), alifariki dunia katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo kutokana na kuumwa kichwa ghafla.
MUME ASIMULIA
Akizungumza na Amani lililofunga safari kutoka Dar hadi Bagamoyo, mume wa Tunu, Iddi Ramadhani alisema mkewe alianza kupata maumivu ya sikio baadaye kichwani ambapo alimhamishia kwa wazazi wake maeneo hayohayo ya Magomeni kwa kuwa ni karibu na hospitali.
Iddi alisimulia kuwa Juni 27, mkewe huyo alipelekwa kwenye hospitali hiyo, akatundikiwa dripu lakini hali ilizidi kuwa mbaya kiasi cha kuwekewa mashine ya kupumulia kabla ya kuaga dunia alfajiri ya Juni 28.
“Baada ya daktari kuthibitisha kifo cha mke wangu, ndugu tulikutana, tukaandaa mazishi kwa kuchimba kaburi na shughuli ya kuandaa maiti kwa ajili ya mazishi tuliyopanga yafanyike saa 6:00 siku ya pili yake yaani Juni 29.
“Wakati wa kuosha maiti mara tukasikia sauti kasha ikafumbua macho, miguu yake ikajinyoosha na mwili ukawa na joto.
“Ilibidi tusitishe kumzika kwanza na kujaribu kumtafuta daktari,” alisema Idd.
Aliongeza kuwa, hali ya marehemu iliendelea kuwatatiza kwa kuwa wataalam walishindwa kufanya chochote hadi Juni 29, walishangazwa zaidi kuona maiti ikiwa inatoka jasho jingi huku joto likiendelea kuwa vilevile.
SHEHE ANENA
Akizungumza na waandishi wetu, shehe aliyekuwa akisimamia kuandaa maiti, Mtawa Adam (pichani) alisema kuwa kwa mujibu wa taratibu za mazishi za Dini ya Kiislam, marehemu ambaye ni mwanamke huoshwa na wanawake wenzake, kanuni ambayo mwili wa Tunu nao uliipitia.
Shehe Adam alisema kuwa, kama kawaida alimpima marehemu na kumshonea sanda huku akisubiria wanawake hao wamalize kumuosha na kumuandaa ili yeye aingie kwa ajili ya kumnyosha viungo, lakini kabla hawajamaliza, alishtushwa kuwaona wakitoka mbio na kudai maiti imefumbua macho na kunyoosha mguu.
“Niliingia ndani na kumuona marehemu ambapo wakati huo alikuwa amefumba macho, nilipomgusa alionekana wa moto kama alikuwa hai, nikamtazama nyayo zake zilionekana ni nyeupe tofauti na za marehemu ambazo huwa za njano.
“Nilimrekebisha mguu wake aliounyoosha, lakini nikashangaa ukirudi tena kama ulivyokuwa awali na hata mapigo yake ya moyo yalikuwa yakipiga mara moja baada ya dakika hata mbili,” alisema shehe huyo na kuongeza kuwa aliwashauri wanafamilia wamuondoe Tunu kwenye kitanda cha maiti na kughairi maziko huku daktari mwingine akiitwa kumpima lakini naye alisema alifariki dunia.
UMATI WAJAA
Waandishi wetu, walishuhudia umati wa waombolezaji wakiwa wamezunguka eneo hilo ili kushuhudia kilichoendelea.
MAMA APANDISHA MASHETANI
Katika hali isiyo ya kawaida, mama mmoja alipandisha mashetani na kudai Tunu hajafa.
WAGANGA WANNE
Kwa mujibu wa ndugu mmoja wa familia hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, waliwaita waganga wa nne wa kienyeji ambapo mmoja alifika na kudai Tunu alichukuliwa msukule lakini alishindwa kumfanya awe hai.
Aidha, waganga waliobakia licha ya kufanya ndumba zao, Tunu hakuweza kuamka kama walivyodai awali.
Baba mzazi wa marehemu, Adam Hassan akizungumza na waandishi wetu alisema Tunu hakuonesha dalili za kuwa hai hivyo taratibu za mazishi zilifanyika kesho yake (Juni 30) na kuzikwa katika Makaburi ya Kiwangwa, Bagamoyo.

AJALI YA BASI NA TRENI YAUA 5 NA KUJERUHI 24 WILAYANI KILOSA


Maofisa wa usalama barabarani wakichukua taarifa eneo la ajali.
Coaster baada ya kuigonga treni.
Wananchi wakishuhudia ajali hiyo.
WATU watano wamepoteza maisha huku 24 wakijeruhiwa baada ya basi la abiria kuligonga treni lililokuwa linatoka Morogoro – Dodoma leo asubuhi katika eneo la Kibaoni, wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
Basi lililohusika katika ajali hiyo ni aina ya Isuzu Coaster lenye namba za usajili T837 CTM linalomilikiwa na Feisal A. Khuwel wa wilayani Kilosa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa ajali hiyo imetokea leo majira ya saa 1 asubuhi na imetokana na uzembe wa dereva wa basi.
Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wiaya Kilosa, Dickson Masale amethibitisha kupokea miili ya watu watano akiwemo dereva wa basi pamoja na majeruhi 24.

WASTARA: NAMPA BOND NAFASI YA KUNIOA!

WASTARA Juma Issa Abeid amekiri kuzidiwa na hisia za kuwa na mwenza kutokana na ukweli kwamba damu yake bado changa, hivyo suala la kuolewa halikwepeki huku akimpa nafasi kubwa msanii mwenzake, Bond Bin Sinan endapo atakidhi vigezo na masharti.

Wastara Juma Issa Abeid akiwa na Bond.
Akifungulia ‘koki’ ya maneno mbele ya paparazi wetu kwa njia ya simu mwanzoni mwa wiki hii, Wastara ambaye kwa sasa yuko bize kusaka ubunge nyumbani kwao Morogoro Vijijini, alisema hawezi kudanganya kwamba ataishi bila kuwa na mume kwa kuwa amekamilika kimaumbile.
“Mimi ni mwanamke, nimekamilika tena nakula na ninashiba. Damu bado changa. Nikisema siwezi kuolewa, nitakuwa nadanganya. Nimekaa muda mrefu kwa sababu kila mwanaume anayenihitaji ananitamani tu.
“Bond namuona ni mwelewa. Lakini nimempa sharti la kutonigusa hadi siku ya ndoa. Kama atakidhi na hayo mengine ambayo ni siri yetu, niko tayari kuolewa naye,” alisema Wastara.

ESTER AZIDI KUTESWA NA TUMBO LA BIA!

KUNENEPEANA! Kuvimbiana na kuongezeka kwa ukubwa wa tumbo kunazidi kumpa wakati mgumu msanii ‘anayechungulia’ katika gemu la uigizaji, Ester Kiama kufuatia kusongwa na madai kuwa ‘amebugia kijusi’ (mjamzito) huku Kulwa Kikumba ‘Dude’ akidaiwa kuwa baba kijacho.

Msanii ‘anayechungulia’ katika gemu la uigizaji, Ester Kiama.
Akikutanisha ‘lips’ na paparazi wetu hivi karibuni, Ester alisema licha ya kuwaeleza watu kwamba ukubwa wa tumbo lake unatokana na utumiaji wa vinywaji vyenye ngano (kama bia) na uvivu wa kufanya mazoezi, lakini wao wamekuwa wakimkomalia kuwa ni mimba.
“Watu wengi wanasema nina mimba. Wengine wanakwenda mbele zaidi wakinipongeza kwa kumbebea mimba ya Dude. Yaani napata wakati mgumu,” alisema Ester.

BAADA YA KUACHANA NA MUMEWE, ROSE NDAUKA APEWA ONYO NA FAMILIA!

Staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka.

STAA wa filamu Bongo, Rose Ndauka hivi karibuni amewekwa chini na familia yake na kupewa onyo kuhusu wanaume pamoja na maadili.
Kwa mujibu wa chanzo, Rose aliambiwa maneno mengi na familia yake ikimtaka ajirekebishe na haswa ajitume zaidi katika kazi zake anazofanya.
“Familia yake imeamua kumuweka chini na kumwambia mengi kuhusu maisha haswa ikimtaka ajirekebishe tabia yake kwa ujumla,” kilisema chanzo.
Rose alipotafutwa kuweka wazi juu ya hili, alifunguka;
“Kila familia ina utaratibu wake, kwahiyo mimi kuwekwa na familia na kupewa onyo wala siyo suala la ajabu.”

BAADA YA MSANII WOLPER KUKIRI YEYE NI FREEMASON, WENYEWE FREEMASON WAMJIA JUU!

KATIKA toleo lililopita la gazeti hili, ukurasa wake wa pili kulikuwa na habari yenye kichwa; Wolper: Mimi ni Freemason kwa muda mrefu sasa.
Sasa, baada ya habari ile kutoka, kuna madai kwamba, wenyewe Freemason wameingiwa na wasiwasi juu ya kauli ile lakini chanzo kikitoa kauli mbili tofauti.
Chanzo chetu kililiambia gazeti hili kuwa, baadhi ya wanachama wa taasisi hiyo wameshtushwa na maneno ya Wolper kama yana ukweli wowote.
“Yaani kule Freemason, baachi ya wanachama wanasema Wolper alikurupuka kusema vile. Lakini hawajasem alikurupuka kwa sababu si Freemason au hakutakiwa kukiri,” kilisema chanzo.
Jumatatu iliyopita, Amani lilimpigia simu mwanachama mmoja wa taasisi hiyo ambaye yupo ngazi ya uongozi na kuzungumza naye kuhusu Wolper lakini alikata simu bila kutoa majibu.
Wolper mwenyewe alipotafutwa kwa simu na kuulizwa kama anajua ameibua kizaazaa hicho, alijibu ndivyo sivyo:
“Mimi niko mbali na mji jamani. Nina mishemishe f’lani hivi. Unajua nataka kutoa filamu. Nitakuja siku moja hapo Global kuomba udhamini wa filamu hiyo.”
Staa wa filamu Bongo, Jackline Wolper.
Sasa, baada ya habari ile kutoka, kuna madai kwamba, wenyewe Freemason wameingiwa na wasiwasi juu ya kauli ile lakini chanzo kikitoa kauli mbili tofauti.
Chanzo chetu kililiambia gazeti hili kuwa, baadhi ya wanachama wa taasisi hiyo wameshtushwa na maneno ya Wolper kama yana ukweli wowote.
“Yaani kule Freemason, baachi ya wanachama wanasema Wolper alikurupuka kusema vile. Lakini hawajasem alikurupuka kwa sababu si Freemason au hakutakiwa kukiri,” kilisema chanzo.
Jumatatu iliyopita, Amani lilimpigia simu mwanachama  mmoja wa taasisi hiyo ambaye yupo ngazi ya uongozi na kuzungumza naye kuhusu Wolper lakini alikata simu bila kutoa majibu.
Wolper mwenyewe alipotafutwa kwa simu na kuulizwa kama anajua ameibua kizaazaa hicho, alijibu ndivyo sivyo:
“Mimi niko mbali na mji jamani. Nina mishemishe f’lani hivi. Unajua nataka kutoa filamu. Nitakuja siku moja hapo Global kuomba udhamini wa filamu hiyo.”

HUYU NDIYE MSANII WA BONGO ALIYEKIRI KUTESWA NA MAPENZI KWA SABABU YA UNENE WAKE!

Mtangazaji wa ITV / Radio One, Farhia Middle.
MTANGAZAJI wa ITV / Radio One, Farhia Middle amesema tangu aujue ulimwengu wa mapenzi hajawahi kukutana na mwanaume mwaminifu na kwamba kila mara amekuwa akilizwa na mapenzi jambo ambalo husababisha kujiona mwenye mkosi.
Akipiga stori na gazeti hili hivi karibuni, mtangazaji huyo alisema licha ya baadhi ya watu kumsifia kuwa ni mrembo kwa sura na umbo, lakini amekuwa akikutana na balaa la kuumizwa na mapenzi kwa kusalitiwa ama kunyanyaswa na wanaume.
“Yaani huwezi amini, wakati mwingine huwa najiuliza kwa nini mimi? Mbona kila mwanaume ninayempata sidumu naye. Kama siyo msaliti basi ni yule mwenye mfumo dume na hulka za kunyanyasa. Najiona kama nina mkosi,” alisema Farhia.

PICHA ZA ZISIZO NA MAADILI ZA MREMBO HUYU ZAMUUA BABA YAKE!


Loredana Chivu ni mwanamitindo nchini RomaniaBaba mmoja amejiua baada ya kuona picha za uchi zamwanawe wa kike katika jarida la Playboy nchini Romania.
Loredana Chivu alirarua ukurasa uliokuwa na picha yake akiwa 'amepos' katika jarida hilo la Playboy na punde babake alipogundua kuhusu picha hizo, alizongwa na mawazo na hata kumkana mwanawe.
Kwa mujibu wa mtandao wa Mirror, msichana huyo mwenye umbo la kuvutia alisema, '' babangu aliacha kuongea na mimi na kuonekana mwenye hasira sana''.

"alipogundua kuwa picha hizo zilikua zangu, alijitenga sana na kujaribu kunitenga na mimi''.
Nilidhani labda angesahau na sikudhani hata siku moja angejitoa uhai. Loredana Chivu anasema anajuta sana kwani babake hakuwahi kuongea naye baada ya kupata picha zake.
Mwanamitindo huyo Loredana Chivu mwenye mamia ya picha akiwa nusu uchi kwenye akaunti yake ya Instagram, alikuwa na uhusiano wa karibu sana na babake lakini alisema yote hayo yalibadilika baada ya babake kuona picha zake akiwa nusu uchi.
Alipokwenda kumtembelea babake miezi michache baadaye, baada ya kuamua kwamba kimya kilikuwa kimeendelea kwa muda mrefu sana, alishtuka sana kumpata babake akiwa amejitoa uhai
"nilipata akiwa na kamba shingoni akiwa ananing'inia chumbani''.

Loredana,anayeishi nchini Romania, anasema kuwa tangu kifo cha babake, amekuwa akiwaza na kuwazua kwamba aliamua kujiua kwa sababu ya mgogoro kati yetu na hasa kuhusu picha zangu zilizoziona kwenye jarida la Playboy.
''Najuta sana kwamba hakuwahi kupata muda wa kuzungumza na babangu kuhusu yaliyotokea''.

''Hakuwacha ujumbe wowote kabla ya kujitoa uhai, siku zote tulikuwa na uhusiano mzuri lakini yote yalibadilika baada ya baba kuona picha zangu nikiwa uchi. Bado inaniuma sana na singemtakia mtu yeyote kupatwa na kama yaliyonikuta''.


-BBC SWAHILI

MJUE MODEL MKALI MWENYE FOLLOWERS WENGI SANA HUKO INSTA

Anaitwa Kathy...kutoka CUBA




HIVI DADA ZETU MNAPOPIGA PICHA KAMA HIZI MNAKUA MNATAKA NINI??!! WATAZAME HAWA



 

 

UJAUZITO UMENIVURUGA SHEPU YANGU, TIWA SAVAGE

Mwanamuziki wa Nigeria,  Tiwa Savage.
Lagos Nigeria
MWANAMUZIKI Tiwa Savage wa Nigeria amelalamika kwamba ujauzito alio nao hivi sasa umevuruga shepu yake hasa kutokana tumbo kujitokeza.
Tiwa Savage akiwa na mumewe Tunji ‘Teebillz’ Balogun.
Mrembo huyo ambaye anategemea kumzalia mtoto  mumeweTunji ‘Teebillz’ Balogun, amesema kwenye akaunti yake ya Instagram kwamba pamoja na kufurahia hali hiyo, ujauzito una changamoto zake.
“Wakati wote unatamani uzae mtoto umwona na unakuwa unafurahi wakati anapojitingisha tumboni na unapofahamu kwamba sasa amelala.”Ni safari ya kufurahisha tangu ujauzito hadi mwisho wake,” aliandika.

MWALIMU SEKONDARI AKAMATWA NA ‘UNGA’

Na Makongoro Oging’
Mwalimu wa shule moja ya sekondari mkoani Singida (jina la shule linahifadhiwa), Charles Andrew (46) amekamatwa na Kikosi Kazi cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya nchini (task force) katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere akidawa kuwa na mzigo wa ‘unga’ pipi 101 ya aina ya heroin yenye zaidi ya shilingi milioni mia moja.

Mwalimu wa shule moja ya sekondari mkoani Singida (jina la shule linahifadhiwa), Charles Andrew (46) anayedaiwa kukamatwa na unga.
Taarifa kutoka vyanzo vyetu makini ndani ya kikosi hicho zinasema kwamba mwalimu huyo alikamatwa Juni 25, mwaka huu, saa kumi alfajiri akijianda kusafiri kwenda nchini Ghana kupitia Nairobi.
Habari zaidi zinadai kwamba mwalimu huyo alipokamatwa alikutwa na pipi 40 akiwa amezificha sehemu za siri na baadaye alitoa pipi 61 ambazo alimeza tumboni.


Kamanda wa Polisi Kikosi cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa alipoulizwa ofisini kwake na mwandishi wetu juzi alikiri kukamatwa kwa mtu huyo na kiasi hicho cha madawa.
“Tulipata taarifa kutoka kwa raia mwema ndipo tukaweka mtego na tukafanikiwa kumkamata mtu huyo ambaye kitaaluma ni mwalimu wa shule ya sekondari huko mkoani Singida, hata hivyo tutamfikisha mahakamani wakati wowote upelelezi ukikamilika,” alisema Kamanda Nzowa.
Kamanda Nzowa amewashukuru wananchi kwa ushirikiano wanaotoa juu ya wauza na watumiaji wa unga na waendelee kushirikiana na polisi ili kukomesha kabisa biashara hiyo haramu.

INASIKITISHA SANA..!! DENTI KIDATO CHA KWANZA AFIA BWAWANI!

Na Kulwa Mwaibale MSIBA! Mohamed Juma (14) ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Shule ya Sekondari ya Toangoma wilayani Temeke, Dar amefia bwawani wakati akiogelea.
Tukio hilo lililoacha majonzi kwa ndugu, jamaa, marafiki na wanafunzi wenzake, lilijiri Juni 26, mwaka huu, majira ya alasiri.

Mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Shule ya Sekondari ya Toangoma wilayani Temeke, Dar, Mohamed Juma (14) amefia bwawani wakati akiogelea.
Akizungumza na Uwazi kwa masikitiko makubwa ya kumpoteza mwanaye, baba mzazi, Juma Shaha alisema familia yake imepata pigo kubwa kwa kuondokewa na mtoto wao wa kiume.
“Nashindwa nianzie wapi kuzungumza maana tumepata pigo kubwa sana kuondokewa na mwanangu wa kwanza katika uzao wetu wa watoto watatu wa kiume, inauma sana kwa kweli,” alisema Juma.
Juma alisema, majira ya saa 4 asubuhi ya siku ya tukio, Mohamed aliaga  kwenda twisheni na baadaye saa 8 kuelekea 9 alasiri alikwenda kwa rafiki zake Kilakala, Kongowe.
“Jambo la kushangaza, hadi inafika saa 2 usiku, Mohamed hakuonekana nyumbani ndipo tulianza kumtafuta,” alisema mzazi huyo.
Baba Mohamed alisema alikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Kongowe ambapo walimweleza aendelee kumtafuta.
Aliongeza kuwa, baada ya hapo alikwenda kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Tuangoma ambaye aliungana naye kumtafuta bila mafanikio.
Juma alisema kuwa, licha ya kutoa taarifa Polisi Kongowe, alishauriwa kuripoti pia Kituo Kikuu cha Polisi Mbagala-Maturubai.
Alisema, wakati akirejea nyumbani kutoka kituoni, mkewe, Rahma Juma alimpigia simu na kumfahamisha kwamba rafiki zake Mohamed  walipeleka nguo za marehemu nyumbani.
Aliendelea kusimulia kuwa, walipowahoji watoto hao, Gabriel na Musa walisema wakati wakijiandaa kuogelea kwenye bwawa hilo lililopo Toangoma, walimuona nyoka mkubwa ndipo walichukua nguo na kukimbia wakimuacha Mohamed.
Mzee huyo alisema walipokwenda Toangoma alikokutana na Mkuu wa Sekondari ya Toangoma, Nchimbi na vijana kadhaa wakaenda kwenye bwawa hilo.
Walipofika, vijana wanaoweza kuogelea walijitosa kwenye bwawa kumtafuta Mohamed ambapo walifanikiwa kumuibua akiwa amenasa kwenye matope huku ameshafariki dunia.
Mzazi huyo alisema kwamba, katika jambo la kushangaza, Mohamed hakunywa maji kama inavyokuwa kwa watu wanaokufa vifo vya ajali ya maji.
“Baada ya polisi kufika walinihoji nikawaeleza kisa cha mwanangu kufariki dunia ndipo wakauchukua mwili kwenye gari na kuupeleka nyumbani kwangu, tukafanya taratibu za mazishi na kumzika katika Makaburi ya Kimicha yaliyopo hukuhuku Kongowe,” alisema Juma kwa huzuni

INASIKITISHA: FAMILIA YATUPIWA YATUPIWA VYOMBO NJE!


Shani Ramadhani na Mayasa Mariwata
USIOMBE yakukute! Beatrice Nyato au mama Prisca, mkazi wa Kurasini, Dar, anapika, anapakua na kulala nje ya nyumba yake baada ya kutupiwa vyombo nje na mtu aliyemtaja kwa jina moja la Anwar ambaye ni mkurugenzi wa kampuni moja ya usafirishaji ya jijini Dar.

Beatrice Nyato au mama Prisca, mkazi wa Kurasini, Dar, anayepika, anapakua na kulala nje ya nyumba yake.
Akizungumza na Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita, mama Prisca alisema kasheshe hiyo ilimkumba yeye na wapangaji wake.
Alisema awali alikwenda katika ofisi za mkurugenzi huyo kwa lengo la kuuza nyumba yake ili amlipie mume wa binti yake deni la benki ambapo yeye ndiye alimdhamini kupitia nyumba hiyo.

Vitu vya familia hiyo vikiwa nje ya nyumba.
“Nilisikia ile kampuni huwa inanunua nyumba. Nilipofika, tukaongea na mkurugenzi, akanipa mtu nije naye ili aione. Nyumba yangu ni kubwa, ina vyumba kumi na sehemu ambayo unaweza kupaki magari madogo hata kumi.
“Yule mtu alipoiona akaenda kumwambia bosi wake, kesho yake naye akaja kuiona.  Kuhusu bei, nilimwambia Sh. milioni 600, yeye akasema parefu. Nikashuka hadi Sh. milioni 500, akasema atanipa Sh. milioni 400 lakini baadaye akasema atanipa milioni 320 ili milioni 80 iwe kwa ajili ya kuhamisha wapangaji, bili ya maji na umeme. Nikakubali,” alisema mwanamke huyo.
Mama Prisca alisema, waliandikishiana kwenye karatasi kwa makubaliano ya kuanza kulipa pesa anazodaiwa benki, zinazobaki kumlipa kupitia cheki.
Bosi huyo, kwa mujibu wa mama Prisca, aliahidi kuanza kulipa shilingi milioni 150 kwa ajili ya benki (jina lipo) na nyingine angemalizia baadaye.

Prisca, mkazi wa Kurasini, Dar, akipika nje ya nyumba yake.
“Siku kadhaa mbele alinipigia simu akasema atanipa afisa niende naye benki kwa ajili ya kufuatilia hati kwa kuwa yeye atakuwa safirini. Nikaambiwa mimi na mkwe wangu tuandike barua iende benki.
“Baada ya wiki mbili nikapigiwa simu na benki kuwa deni la Sh. milioni 50 limeshalipwa.
“Kulikuwa na deni la pili, benki nyingine, mkurugenzi akasema hawezi kulipa bila mimi kutoa hati ya nyumba, nikampa, akalipa benki Sh. milioni 70,” alisema mama huyo.
Mama Prisca alikuwa akiendelea kudai Sh. milioni 80 ambayo walikubaliana ilipwe kupitia cheki lakini alipokwenda kwa ajili ya kujaza fomu ili aingiziwe fedha yake hiyo alishangaa kuambiwa malipo yameishia pale na hakuna zaidi ikiwa na maana kwamba, nyumba ilinunuliwa kwa Sh. milioni 270  tu!
 “Nilimfuata tena, akaja juu, akasema nataka nini tena? Huku akinitolea maneno makali kuwa yeye ni mgonjwa nampigia kelele, akasema niondoke asije akaniitia polisi.


“Hivi karibuni, sijui siku gani ile! Saa 5:00 asubuhi, walikuja watu waliojitambulisha kuwa wanatoka kampuni ya udalali wakiwa wameongozana na mabaunsa kama 10 na askari 15, wakadai wametumwa na aliyenunua nyumba kuibomoa.
“Mimi sikuwepo, hata wapangaji walikuwa kwenye shughuli zao, lakini kaka yangu alikuwepo. Aliwazuia kwa kuwataka waende kwanza serikali za mtaa lakini wakagoma.
“Kaka alinipigia simu na kunipa taarifa, nikachanganyikiwa, nikakumbuka nina fedha ndani, nikamwambia atoe mfuko wenye fedha, akasema haupo ila mimi nifanye ninavyoweza niwahi.
“Nilipofika, niliwakuta mabaunsa na polisi wenye silaha wameizingira nyumba. Nikazuiliwa kuingia kwa kuambiwa kuna kazi inaendelea.
“Majirani zangu wakaja kunivuta pembeni na kuniambia mama Prisca utazimia utupe kazi ya kukupepea au utakufa kwa presha. Nikakaa pembeni wakinipepea, baadaye wakaniondoa kabisa eneo lile.
“Wakati naondoka, nikampigia simu wakili wangu, akaniambia suala langu linatakiwa lifikishwe mahakamani. Mpaka leo ni siku ya 10, tunalala hapa nje, ndani kuna walinzi wenye silaha, wanaingia kwa shifti. Geti limefungwa na mnyororo.
 “Wapangaji nao baada ya kukuta vyombo vyao vipo nje wakapaniki, wakasema watanipiga vinginevyo niwape fedha ya kulala gesti na fedha ya chakula. Jumanne iliyopita wakanipeleka Kituo cha Polisi Chang’ombe, nikalala siku moja, siku ya pili nikapelekwa Kituo cha Polisi Kilwa Road nikalala, kesho yake nikatolewa kwa dhamana.
Baada ya kutoka kwa mama Prisca, waandishi wetu walikwenda kwenye ofisi za mkurugenzi huyo zilizopo Kurasini ambapo walinzi waliwazuia kuingia ndani wakidai hairuhusiwi.
Jumamosi iliyopita, waandishi wetu walikwenda tena lakini mtu mmoja aliyekataa kujitambulisba alisema ishu ya mwanamke huyo ipo polisi (bila kutaja kituo) hivyo mkurugenzi huyo hawezi kusema lolote na hakukuwa na kiongozi yeyote ofisini hapo.

MTOTO WA WAZIRI ATUHUMIWA KWA KUUA!

Deogratius Mongela na Chande Abdallah INASIKITISHA! Mmiliki wa Shule ya Msingi na Awali (International) ya Mount Zion iliyopo Bahari Beach, Dar, Annah Mizighi Mwambili, 47, (pichani) ameuawa na mwili wake kutupwa ndani ya shule yake baada ya kupotea kwa zaidi ya miezi sita huku mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi akidaiwa kuwa mmoja kati ya watuhumiwa wa mauaji hayo.
Mmiliki wa Shule ya Msingi na Awali (International) ya Mount Zion iliyopo Bahari Beach, Dar, Annah Mizighi Mwambili enzi wa uhai wake.
Duru za awali za upelelezi wa polisi, zinamtaja Said kuwa alikuwa na uhusiano wa karibu na marehemu bila kufafanua alihusikaje na mauaji hayo ya kinyama yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana, siku na tarehe isiyojulikana na mwili wake kutupwa kwenye shimo la maji taka ndani ya eneo la shule aliyokuwa akiimiliki.
Aidha, nyuma ya taarifa hiyo ya mauaji, deni la shilingi milioni mia tisa (900,000,000) ambalo mwanamke huyo alikuwa akimdai mmoja kati ya watuhumiwa hao ambao majina yao yote bado hayajafahamika likitajwa kuwa ndiyo chanzo cha Annah kutolewa uhai.

ALIANZA KWA KUTOWEKA
Wakisimulia kwa uchungu namna Annah alivyotoweka nyumbani kwake, ndugu wa marehemu walisema, awali Desemba 26, mwaka jana kwenye Sikukuu ya Boxing Day, kuna wageni walifika nyumbani kwake, Boko, Dar, wakazungumza na baadaye wakaondoka naye na hakurudi tena.

Mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi anayedaiwa kuwa mmoja kati ya watuhumiwa wa mauaji hayo.
NDUGU WAPATA WASIWASI, WATOA TAARIFA POLISI
Ndugu hao walisema kuwa siku za kwanza hawakupata wasiwasi kwa vile ilikuwa kawaida ya marehemu kuwa mtu wa safari kutokana na biashara zake na kuongeza kuwa walianza kupata wasiwasi baada ya siku nne kupita huku kukiwa hakuna mawasiliano kati yao na marehemu, jambo lililowalazimu kuripoti Kituo cha Polisi cha Wazo Hill ambao walianza uchunguzi.

WAUMINI WAFUNGA NA KUSALI
Wakati wote huo, waumini wa kanisa alilokuwa akisali marehemu Annah la Winners Chapel lililopo Ukonga jijini Dar waliamua kufanya maombi ya kusali na kufunga kwa ajili ya kumuomba Mungu awaoneshe  mpendwa wao alipo.

MAITI YAPATIKANA SHULENI KWAKE MIEZI 6 BAADAYE
Kwa masikitiko makubwa, ndugu hao walisema, Juni 22, mwaka huu, ikiwa ni miezi sita na siku na chache tangu kupotea kwa ndugu yao, walipata taarifa iliyowashtua na kuwaumiza, kwamba mwili wa mpendwa wao umepatikana ukiwa umeharibika vibaya ndani ya shimo la maji machafu katika shule yake.

Ndugu, jamaaa na marafiki wakiwa katika misa ya mazishi.
HABARI ZA CHINICHINI
Habari za chinichini ambazo si rasmi zilizonyakwa na Gazeti la Uwazi, zinaeleza kuwa baada ya marehemu huyo kuchukuliwa nyumbani kwake, inadaiwa watuhumiwa walikwenda naye mpaka kwenye nyumba ya mganga mmoja maarufu wa kienyeji (jina kapuni) ambako walimuua kisha kuuchukua mwili wake na kuutupa shimoni.

POLISI WANASA TUKIO
Kama Waswahili wasemavyo, damu nzito kuliko maji ndivyo ilivyokuwa kwa Annah ambaye damu yake iliendelea kuwasumbua wahusika kiasi cha unyama wao kuwafikia polisi kupitia njia za kijasusi na hivyo kufanikiwa kumnasa mmoja wa watuhumiwa.
“Polisi walipopata taarifa za mauaji hayo, waliamua kufuatilia, wakabaini mmoja kati ya watuhumiwa hao yuko Arusha. Wakamuwekea mtego na kufanikiwa kumnasa, wakamleta jijini Dar ambapo aliwataja aliodai kushirikiana nao,” chanzo kutoka vyombo vya usalama kililiambia Uwazi.

MWALIMU MKUU AZUNGUMZA
Akizungumza na Uwazi, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Dony Maige alisema shule yake ilikuwa imefungwa wakati marehemu ambaye ni mmiliki na mkurugenzi akiwa hajulikani alipo.
“Januari mwaka huu, tarehe za mwanzoni tulifungua shule kama kawaida baada ya likizo ya Desemba ambapo wanafunzi waliendelea na masomo. Lakini bajeti ilikuwa ngumu kutokana na mkurugenzi ambaye ndiye mtoaji wa fedha za matumizi ya shule na malipo ya wafanyakazi, kutoonekana.
“Hali hiyo ilisababisha baadhi ya wazazi kulazimika kuchangia huduma nyingine muhimu japokuwa walikuwa wamemaliza ada za watoto wao.

MWALIMU AWATOA MACHOZI WAOMBOLEZAJI
“Juni 21, mwaka huu tukiwa tumefunga shule na kutarajia kufungua tena kwa ajili ya muhula mpya wa masomo, ndipo nilipopokea simu kutoka vyombo vya usalama na kunitaka kusitisha zoezi la kufungua shule kwa kuwa kutakuwa na oparesheni maalumu katika eneo la shule. Nikaambiwa niwaondoe wafanyakazi wote isipokuwa mimi peke yangu.
“Nilishangaa, baada ya kufika shuleni na kuwaona polisi wakiwa eneo la tukio. Nilishtuka kutokana na maswali waliyokuwa wakiniuliza. Lakini jambo lililonishtua zaidi ni kuuona mwili wa marehemu Annah ukitolewa ndani ya shimo la maji machafu lililopo ndani ya shule ambayo kwa miezi yote sita wanafunzi na hata sisi walimu tulikuwa tukipita bila kujua.
“Kwa kweli sijawahi kukutana na kipindi kigumu kama hiki katika maisha yangu. Ni jambo la ajabu sana. Nimejiuliza maswali mengi na kukosa majibu,” alisema mwalimu huyo huku waombolezaji wakishindwa kuzuia machozi yaliyokuwa yakiwatiririka.

MWILI WAAGWA BILA KUFUNULIWA
Wakati wa kuuaga mwili huo, Jumamosi iliyopita nyumbani kwa marehemu, waombolezaji walitoa heshima zao za mwisho kwa masikitiko mbele ya jeneza la marehemu bila kufunuliwa kutokana na mabaki ya mwili huo kuharibika vibaya.
Mwili wa marehemu Annah ulipumzishwa katika Makaburi ya Kwakondo, Ununio jijini Dar. Hakika bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina lake libarikiwe. Amina. Marehemu ameacha watoto watatu, Steven, Irene na Emerly Mwambili.

POLISI KINONDONI WALIVYOSEMA
Uwazi lilimpigia simu Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP Emanuel Mlei na kumuuliza yafuatayo.
Uwazi:  “Kuna madai kwamba, mtoto wa aliyewahi kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya tatu, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi mnamshikilia kwa mauaji ya mwanamke aliyekuwa mmiliki wa shule, Annah Mwambili, ni kweli?”
Kamanda: “Kuhusu hilo siwezi kulisema kwa sasa. Ila kesho (jana) nenda pale kwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Suleiman Kova ataliongelea yeye.”
Uwazi bado liko kazini kuchimba tukio hili la kinyama na kwamba litaendelea kuwaletea mapya kadiri yanavyopatikana.
Older Posts
© Copyright ZEE LA UDAKU | Designed By Code Nirvana
Back To Top