Habari Kali
Loading...

HII NDIO KAULI YA SALAMA JABIR NA SOLO THANG KWENDA KWA MASHABIKI WA ALI KIBA NA DIAMOND!

SalamaUpinzani unaokuzwa na mashabiki kati ya Diamond Platnumz na Ali Kiba kwenye mitandao ya kijamii umepelekea Mastaa wa Tanzania kuanza kujitokeza hadharani na kuwaweka mashabiki hawa sawa kwa kuamini wamevuka mipaka kwenye ushabiki.
Mtangazaji wa TV show ya Mkasi Salama Jabir na msanii mkongwe bongoflevani Solo Thang ni miongoni mwa waliozipaza sauti zao June 30 2015.
Kupitia kwenye ukurasa wa twitter Salama Jabir aliandika ‘Wabongo tumekua wakosoaji mpaka wasanii wanajishtukia, hakuna “zuri kabisa” kwenye macho yetu… tuwaache wasanii wawe “Wasanii” nadhani!
.Jana tulikua tunaongea na wana job, Ali Kiba hakuwa mtu wa vioo vikali, yeye alikuwa anatoa audio kali na video ya Mwananchi kamaliza, zama zimebadilika mpaka anakwea pipa kwenda kutoa kideo kikaaali tushukuru, kapendeza, rangi nzuri! mengine tuyaache..’  kauli ya Salama Jabiri
.Upinzani huo ulioanzishwa na makundi yanayojiita (TeamAliKiba na TeamDiamond) yalimkwaza pia mkongwe wa Hip Hop Solo Thang na kuandika..’Ukiweka habari au picha au muziki wa msanii muyu mashabiki  wa yule wanakutukana!  kwanini? ? hii burudani tu isiwe uhasama, tujivunie sanaa yetu..’
solo 1
Solo Thang

DIAMOND KUSHTAKIWA, BAADA YA KUWATELEKEZA WATOTO ALIOAHIDI KUWASOMESHA

Waandishi wetu STAA wa muziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnumz’ ambaye aliwatelekeza watoto wawili alioahidi kuwasomesha katika shule ya East Africa International ya Mikocheni jijini Dar es Salaam, atashtakiwa mahakamani endapo wazazi wa vijana hao wataamua kufanya hivyo, Risasi Mchanganyiko limeelezwa.
Staa wa muziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnumz’.
Meneja wa msanii huyo, Babu Tale, awali aliulizwa na gazeti hili juu ya kinachoendelea kuhusiana na vijana hao waliotimuliwa shule Aprili mwaka huu kwa kutolipiwa ada, lakini akionekana kupatwa na jazba, alisema wanasikitishwa na jinsi wazazi wa watoto hao wanavyokiuka makubaliano, hivyo wao hawataki tena kusema lolote kwa sasa.
“Kama wao wanadhani kwa kwenda kwenye media (vyombo vya habari) ndiyo watoto wao watasomeshwa, basi na waende hukohuko watasomeshewa watoto wao,” alisema Tale aliyeonekana kukasirishwa na mwendelezo wa habari hiyo.
Tale alitoa kauli hiyo kufuatia mmoja wa wazazi hao wa watoto Hillary na Hamis, kudai kuwa hakuna maendeleo yoyote ya kulipiwa ada kwa vijana wao, kwani ingawa waliambiwa mambo yangekuwa sawa baada ya siku chache, lakini danadana zinaendelea.
Mwanasheria mmoja maarufu nchini aliyeomba hifadhi ya jina lake, aliliambia gazeti hili kuwa endapo wazazi wa vijana hao wataamua, sheria zinawaruhusu kumpeleka mahakamani msanii huyo kwa kukiuka mkataba, hata kama haukuandikwa.
“Makubaliano ya mdomo ni mkataba unaotambuliwa kisheria, mradi tu wazazi waweze kuthibitisha, tena kwa hili, inaonyesha siyo tu mkataba, bali inaonyesha Diamond hakufanya hivyo kwa mapenzi yake kwa watoto, bali baada ya wao kumfanyia kitu, aliwapeleka shule kuonyesha u-siriazi aliokuwa nao juu ya ahadi hiyo,” alisema mwanasheria huyo.
Januari mwaka jana, Diamond aliendesha shindano kwa watoto la kucheza mtindo wa Ngololo na kuahidi zawadi kwa washindi katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar. Vijana hao walioshinda, walipewa ofa ya kusomeshwa katika shule hiyo hadi kumaliza elimu yao ya msingi, lakini tangu wapelekwe hawajawahi kulipiwa ada.

DIAMOND ABANWA KUMSALITI MEMBE

Musa mateja
Nimwendo wa kutangaza nia kwa baadhi ya wanasiasa ambao wanaomba ridhaa ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu ambapo upepo huo umemgusa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ baada ya kwenda kufanya shoo wakati Waziri Mkuu Mjiuzulu, Edward Lowassa akitangaza nia mwishoni mwa wiki iliyopita.
Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi, Benardi Memba akiwa na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
TUHUMA ZA USALITI
Mara baada ya Diamond kuangusha bonge la shoo kwenye ‘iventi’ hiyo ya kuanza Safari ya Matumaini ya Lowassa akiungana na wasanii wengine kama Tunda Man, Khadija Kopa, Makomandoo, Nay wa Mitego, Dully Sykes na wengine kibao ndipo madai mazito yakaibuka kuwa amemsaliti mtangaza nia mwingine, Bernard Membe.

TEAM MEMBE MZIGONI
Mara baada ya ishu hiyo, kundi la siri linalojiita Team Membe kwenye Mitandao ya Kijamii ya Instagram, Twitter, Facebook na WhatsApp linalodaiwa kumuunga mkono waziri huyo wa Mambo ya Nje ya Nchi, Memba walianza kutoa vitisho kwa Diamond kuwa watamshikisha adabu kwa kuisaliti kambi yao.“Hakuna asiyejua kama Diamond alikuwa ni Team Membe. Kitendo cha kwenda kumsapoti Lowassa ni usaliti.

ETI WAMETOKA MBALI?
“Sisi (Team Membe) tunajua vitu vingi. Tunajua ukaribu wa Membe kwa Diamond na namna ambavyo amekuwa akimpa sapoti. Ukweli tumeshtushwa kumuona jamaa kwa Lowassa,” ilisomeka sehemu ya maoni ya mmoja wa memba wa Team Membe na kuungwa na mwingine:

Diamond akiongozana na waziri Membe.
“Hata kipindi kile (mwaka jana), Membe alimpa shavu la shoo Mtwara na Lindi na zaidi sana akamkaribisha hotelini wakala chakula pamoja kwa lengo la kujipanga namna ya kusapotiana.“Kuna madai kwamba walikubaliana kwamba Membe atamsaidia kwenye kuupaisha muziki wake kimataifa naye akamuahidi kumsapoti kwenye siasa hasa atakapotangaza nia kwa sababu Diamond ana ushawishi mkubwa ndani na nje ya Bongo.”
WANAMTISHAJE?
Kwa mujibu wa taarifa hizo za mitandaoni, vitisho hivyo vimekuwa vikifanywa kwa maneno tu katika kurasa za Diamond lakini siyo uso kwa uso kwani bado kundi hilo ni la siri.

DIAMOND ANASEMAJE JUU YA SAKATA HILI?
Baada ya kujikusanyia data hizo ambazo ndizo habari ya mjini kwa sasa hasa ikizingatiwa Membe naye atatangaza nia ya kutaka kuwania urais kesho Jumamosi, gazeti hili lilimtafuta Diamond ambapo alitoa waraka mzito:

“Kwanza kabisa watu wanatakiwa kufahamu kwamba mimi sina chama na wala siko upande wowote.
“Yeyote atakayechaguliwa na kuonekana bora kwa wananchi basi mimi kwangu ni sawa maana sina ufahamu mzuri wa siasa kujua yupi anafaa kuliko mwenzake.Lowasa akihutubia kwenye safari ya matumaini.
“Ila wananchi wanatakiwa kufahamu kuwa mimi ni mwanamuziki na kazi yangu ni kuburudisha…hivyo yeyote atakayeniita kwenye hafla yake niburudishe na akafikia matakwa ya malipo yangu basi siwezi kuacha kwenda.“Hivyo nawataarifu wagombea na viongozi wote…mimi ni mwanamuziki wa Tanzania na nipo kwa ajili ya kuwatumikia kiburudani Watanzania wote…. Yeyote atakayetaka nimpatie burudani basi awasiliane na uongozi wangu.”
VIPI KUHUSU VITISHO?
Alipoulizwa juu ya vitisho kutoka kwa kundi lolote, Diamond alisema hajavipata lakini endapo atapata itabidi akaripoti polisi kwa usalama wake.

TUJIKUMBUSHE
Mapema mwaka jana Diamond alialikwa na Membe kwenye shoo za kuhamasisha amani huko Mtwara na Lindi ambapo baada ya shoo alipata fursa ya kula chakula pamoja na mheshimiwa huyo. Huo ndiyo ukawa msingi kwamba staa huyo yupo upande wa Membe.Diamond akitumbuiza.
Hata hivyo, katika maelezo yake, Diamond alikiri kufanya mazungumzo na Membe. Mazungumzo ambayo alidai yalihusu pongezi jinsi anavyojituma na kuitangaza Tanzania.Alisema pia waziri huyo alimuahidi kumpa sapoti kwa kumtafutia shoo nyingi za nje ya nchi huku Diamond yeye akiishia kuisihi serikali kuweka nguvu kwenye Muziki wa Bongo Fleva unaoajiri kundi kubwa la watu.
TUKIRUDI KWA WATANGAZA NIA
Mbali na Lowassa na Membe, wengine ambao wametangaza nia katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni pamoja na Steven Wasira, Mwigulu Nchemba, Profesa Mark Mwandosya, Luhanga Mpina, Profesa Mark Mwandosya, Fredrick Sumaye na wengine kibao.

Bifu kubwa kati ya Diamond na mbunifu mitindo wa Kimataifa toka Marekani...

Mbunifu wa mavazi toka Marekani anaeitwa Roper amelalamika sana kupitia Instagram kwamba Diamond kamuibia design yake... roper anayewavalisha wasanii wakubwa Marekani kama August Alsina, Future, Meek Mill nk ameandika hivi......


" I usually don't blast people who make or wear fakes of my designs but this person went way to far when they used my logo! diamondplatnumz is wearing fake Roperrope shirt made by a person with bad character and a strong lack or originality! This is not ok! If you steal a design please reframe from using the Designers Logo because it's illegalwww.shoproperrope.com''.


Mimi namshauri Diamond na wasanii wengine wa kitanzania kuwa makini na kila kitu wanachofanya haswa kuhusu product wanazotumia coz muziki wa Tanzania sasa unapaa mpaka mbali tofauti na wana vyofikiria...Hapa kuna ishu za copyright, maana kosa alilofanya ni kupost na kutoa credit kwa Desgner wake Qboymsafi pengine bila kujua stylist wake ambae kiukweli bado ajafikia level za kuitwa dizaina (bongo dizaina hakuna bado) alikopi na kupesti dizaini ya mtu mwingine. Inaweza kuwa hana kosa lakini kikinuka yeye ndio atakuwa responsible.

Niliona Adam Mchomvu amekuja na dizain yake ya mavazi aniita Adamz Apple, kiukweli ukiangalia ile dizaini ni copy and paste sasa na huu utandawazi usishangae tukafirisiwa watu huku.

Tuwe makini sana..Na Diamond kama akiweza kukuafford uyu mchizi aongee nae biashara jamaa amtengenezee kazi zake aigeuze hii ni opportunity.

PICHA YA DIAMOND AKILA MISHIKAKI YAZUA GUMZO1

Stori: Musa Mateja PICHA ya staa wa Nasema Nao, Nasibu Abdul ‘Diamond’ inayomuonesha akila mishikika uswahilini imezua gumzo la aina yake mitandaoni.
Staa wa Nasema Nao, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akila mishikika uswahilini.
Picha hiyo ambayo ilipigwa mwaka mmoja uliopita maeneo ya Tip Top, Manzese jijini Dar, imeibua mjadala mpya juzikati kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengine walimpongeza kwa kitendo hicho wengine wakisema si cha hadhi yake.
“Hii ni nzuri kwa mtu kama Diamond akila uswahilini. Anaonesha siyo mtu wa majivuno,” alichangia mdau mtandaoni huku wengine wakidai si sawa kwani anajiabisha.

Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Baada ya chanzo hicho kuipata picha hiyo na kumtumia mwandishi wetu, Mikito Nusunusu ilimtafuta Diamond ili aweze kuizingumzia lakini simu yake haikupatikana lakini Bab Tale alipatikana na kukiri maelezo ya chanzo chetu.
“Hakukuwa na ishu zaidi ya kuitamani mishikaki, tukaona tununue, mbona ni ya toka mwaka jana?,” alisema Bab Tale.

Picha: Diamond amfanyia shopping mwanaye mtarajiwa Uingereza

Diamond Platnumz anajivunia kuwa baba mtarajiwa, ndio maana ameanza mapema kumuandalia mazingira mazuri mwanaye mtarajiwa kwa kumnunulia vitu mbalimbali na kushare na followers wake wa kwenye mitandao ya kijamii.
“Anything for my little angel…” ndio maneno aliyoandika kwenye picha hii.
Muimbaji huyo wa ‘Nasema Nawe’ amabye weekend iliyopita alikuwa na show jijini London, ameshare picha akifanya shopping ya vifaa vya mtoto wanayemtarajia kumpata na Zari The Bosslady.
mondi shopping5
Zari naye alishare picha zingine za Diamond Facebook:
mondi shopping2
“Current situation in London…… damn he thinks ‘she’ should have more than one”-Zari
mondi shopping3
“The excitement tho”– Zari

Campaign ya Ali Kiba Dhidi ya Daimond Platnumz Kill Music Awards..Daimond Adai yeye Sio Size Yao..Atawapelepweta Bure

Licha ya kwamba kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake ila it is not a coincidence ma ex wote wa Mwanamuziki Diamond Platnumz wanafanya campaign za kushawishi watu wampigie kura ally kiba...si kwa vile ni mashabiki wa ally kiba ila ni Figisu Figusu tuu na chuki za mafanikio ya Daimond

Alianza Wema, akaja Jokate na list itaendelea mpaka tukio la utolewaji wa Tuzo hizo... Vitu hivi vyote vinatokea sio kwa bahati mbaya ila watu hao kwa kujua Ally hana uwezo wa kushinda tuzo mbele ya Daimond baasi wameamua kwa makusudi kumfanyia campaign ally ili wafanye revenge ...

Ila uzuri mmoja Mondi bin laden amewaambia kuwa yeye sio size yao..... Atawapelepweta bure

Diamond Platinumz Katika Hili Umekosea,Umekosa Busara ni vyema Ukajifunza Kuweka Akiba ya Maneno

Nime yaandika haya baada ya kuona post ya
Diamond akikosoa vikali tunzo za kill hadi amepitiliza na kuandika yasiyo tarajiwa pengine alikuwa na hasira sana lakini tusisahau kuwa hasira haijengi!
Kwangu mimi naona amekosea sana!

Hakuna busara iliyo kuu kama ku kaa kimya! Hapa ndio naamini wasanii wana hitaji washauri wa karibu kabla ya kuandika au kusema chochote!

Diamond umekosea sana tena sana..ulikuwa na nafasi ya kukaa kimya kuonesha busara kuu!Kuna mtu alisema ukitaka kutambua mtu mwenye busara subiri akiwa na furaha sana au akiwa na hasira sana!

Naanimi Diamond hukufikiri mara mbili kabla ya kupost uliyo yapost! Kila mtu anajua wazi kuwa hizi tunzo hazijakamilika na haziwezi kukamilika kamwe na hata kama kuna mtu atapewa kuziendesha kamwe haziwezi kuwa satisfy watu wote na wakati wote!

Pengine ni kweli anayo jaribu kutuambia Diamond lakini ninacho jiuliza hii ndio busara yako ya mwisho?
Kila mdau wa muziki anajua fika kuwa hakuna mwaka ambao umekuwa na hit song nyingi kama mwaka jana na mimi nilijua utaleta malalamiko mengi sana lakini niliamini kuwa busara ndio itatumika zaidi kuliko hasira au meneno ya kuwa vunja moyo waandaji waonekane hawajafanya lolote kwa kuwa tulio wategemea hawapo!

Diamond una sahau kuwa wakati unapewa tunzo wewe kuna watu wali lalamika kuwa umependelewa na wengine wakajitoa na wengine wakatumia busara na kukaa kimya!

Jamani kama maneno ya namna hii yangekuwa yana andikwa basi yangetoka kwa Bell 9 ambaye watu walikuwa wanaamini kuwa ana stahili tunzo kila leo..lakini kijana wa watu amekuwa ni mwwnye hekima sana na nina mpongeza kwa hilo!

Diamond kusema kuwa hata usipopewa tunzo huwezi kushuka ni kuwakosea heshima Kill na Basata kwani hizi ni tuhumu zisizo na msingi kutoka kwa msanii mkubwa kama wewe ...ni kweli wana lengo la kukushusha?
Diamond umekosa busara kabisa kabisa ulipaswa kukaa kimya maana ni wachache wataamini una watetea hao ulio wataja!

Diamond jifunze kuvumilia na si kila kitu cha kukifanya public..Diamond ina maana kusema kwako hukuhangaika kuwambia watu jinsi ya kupiga kura maana hukupendezwa ina maana umegomea tunzo? Ni kweli Kill na Basata wamekuwa wabaya kiasi hiki hadi una diriki kuuliza kama wanau au kukuza muziki?

Diamond umenishangaza sana tena sana lakini na kukumbusha ujifunze kuweka akiba ya maneno na ndio busara iliyo kuu kuliko kuongea!

Diamond umeshindwa kujiuliza kwanini wengine wame nyamaza?

Mimi naamini hizi tunzo ni nzuri na ni msaada kwa wasanii pia si tunzo zilizo kamilika na hakuna tunzo zilizo kamilika duniani!

Uzuri wasanii huwa mnapewa semina kwa hiyo mnaweza kusema huko huko malalamiko yenu lakini kuongea kwenye media tena kwa njia uliyo tumia itachukuliwa ni kutaka watu wagomee tunzo hizi!

Wasanii ni vyema mkawa mnaweka akiba ya maneno ili msiwa katishe tamaa walio jitoa kuikwamua tasnia hii kwani nao hawaja kamilika!

Karibuni wana jamvi!8

DIAMOND ASAKWA MAZISHI YA BABA WA BABU TALE


Dustan Shekidele, Morogoro BABA mzazi wa Meneja wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Babu Tale, amezikwa juzi Jumanne kijijini kwao Mkuyuni, mjini Morogoro lakini miongoni mwa mambo ya kushangaza ni kitendo cha baadhi ya waombolezaji kumsaka mwanamuziki Nasibu bila mafanikio.
Staa wa Bongo fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Hilo lilijitokeza baada ya msafara uliotokea Dar kufika eneo hilo ambapo vijana walilizingira gari lililokuwa na mastaa na kuanza kuuliza juu ya uwepo wa Diamond.Vijana hao waliotarajia kumuona msanii huyo msibani hapo, hata waliposikia tetesi kuwa hakuwepo, waliendelea kumsaka kila gari huku wakimuuliza kila waliyemuona lakini jibu lilikuwa lilelile, hakufika.
Majibu hayo yalionekana kuwanyong’onyesha vijana hao ambapo baadhi waliamua kuondoka kuonesha dhahiri kuwa kilichowapeleka pale ni kumuona Diamond na si kuzika.Hata hivyo, vijana wengine waliamua kujipoza kwa kupiga picha na Madee kisha kushiriki mazishi hayo mwanzo mwisho.

HUKU DIAMOND AKISUBIRI MTOTO..ZARI NA PEDESHEE KATUNZI WANASWA LAIVU!

Issa Mnally KABAAANG! Wakati supastaa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akitembea kifua mbele huku akijinasibu kuwa anasubiri kwa hamu kupata mtoto kutoka kwa mchumba wake, Zarinah Hassan ‘Zari’, imevuja picha inayomuonesha laivu mwandani wake huyo akiwa na pedeshee maarufu Bongo, Muzamili Issa Katunzi ikidaiwa kuwa ni mtu wake wa nguvu, Ijumaa lina stori kamili.
Zarinah Hassan ‘Zari’ akiwa na pedeshee maarufu Bongo, Muzamili Issa Katunzi.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Katunzi ni mtu wake Zari kitambo kabla hata Diamond hajaanzisha naye uhusiano wa kimapenzi mwishoni mwa mwaka jana na walikuwa wakikutana mara kwa mara.“Katunzi na Zari walijuana kitambo sana. Yaani suala la Zari kuibuka Bongo na kufanya mambo yao haikuwa ishu na hata Katunzi alikuwa akiibuka Sauz (Afrika Kusini anakoishi Zari) na kuwa pamoja,” kilisema chanzo hicho.

KATUNZI ALIWAKUTANISHA ZARI NA DIAMOND
Kuonesha kwamba kina ubuyu kamili, chanzo hicho kilizidi kufunguka kuwa, hata safari ambayo iliwakutanisha Zari na Diamond kwa mara ya kwanza, mrembo huyo alikuja Dar, kumfuata pedeshee Katunzi, ndipo ‘dodo lilipomdondokea’ Diamond kama kumsukuma mlevi vile.

“Kweli Diamond ana zari kama lilivyo jina la mrembo huyo mwenye asili ya Kiganda. Siku hiyo ya kwanza kabisa walipokutana, Zari alikuwa anaibuka Bongo kuitikia wito wa mtu’we Katunzi.
NDANI YA NDEGE SASA
”Diamond alichangamkia fursa, alipoona ‘dhahabu’ inaelea ndani ya ndege katika daraja la  juu (business class), akaomba namba, akakubaliwa na ndipo wakaanza kupiga mapichapicha ya selfie ambayo yalivuja na Wabongo wakaanza kujiongeza kwani wakati huo tayari Diamond alikuwa ameshaachana na Wema Sepetu ‘Madam,” kilitiririka chanzo hicho.

Supastaa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na mpenzi wake Zarinah Hassan ‘Zari’.
PICHA ZAMSHTUA KATUNZI
Kwenye mazungumzo yake, chanzo hicho hakikusita kufunguka kuwa baada ya picha za Diamond na Zari kuanza kuvuja kwa mara ya kwanza, ilidaiwa kuwa zilimshtua Katunzi kiasi cha kumtumia ujumbe mfupi wa simu Zari kumuuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea kati yake na mwanamuziki huyo.“Katunzi ilibidi amuulize Zari kuhusu picha hizo, Zari akamwambia hakuna kitu chochote ni urafiki wa kawaida, hata hivyo jamaa hakujali.

DIAMOND UPOOO!!
“Diamond kama aliingia katika himaya ya Zari pasipo kujua kuna watu wanamjua kitambo atakuwa amechelewa. Pedeshee Katunzi alimjua kitambo sana Zari,” kilimalizia chanzo hicho.

PICHA TOFAUTI ZANASWA
Mbali na kumwaga ubuyu huo, chanzo hicho kilivujisha picha tofauti katika dawati la Ijumaa zinazomuonesha Katunzi akiwa kwenye pozi la pamoja na Zari kuthibitisha kwamba wawili hao ni watu wanaofahamiana.

KWA NINI URAFIKI WA SIRI?
Ijumaa lilifanya uchunguzi wa kwa nini urafiki wa Zari na Katunzi ulikuwa wa siri na kubaini kuwa wawili hao hawakutaka watu wajue kwa sababu ambazo wenyewe wanazijua lakini kitu walichokuwa wanazingatia ni mpango wa ‘kula bata’.
Timu yetu ya uchunguzi imebaini pia kuwa, wawili hao wamekuwa wakiwasiliana mara kwa mara kupitia simu zao za mikononi, mawasiliano ambayo bado yanafanyiwa kazi ili baadaye yapakuliwe yakiwa yameiva.

KATUNZI ANASEMAJE?
Baada ya kumsaka Zari bila mafanikio, mwanahabari wetu alimvutia waya Katunzi ili kumsikia anazungumziaje ukaribu wake na Zari, alipopatikana alijibu kwa kifupi.“Zari namfahamu, kuna nini kwani?” Alihoji  Katunzi. Alipoambiwa kuwa kuna picha na habari zake kuhusu Zari alikata simu na hata alipopigiwa tena hakupokea.

KUTOKA DAWATI LA IJUMAA
Kufuatia kuwepo kwa minong’ono mingi kuhusiana na ukaribu wa Zari na Katunzi, dawati la Ijumaa linaendelea kuchimba undani wa habari hii kwa kumtafuta Katunzi, Zari na Diamond ili wote wafunguke kwa kirefu.

DIAMOND, ZARI NDOA YAFUNGWA RASMI! WENYEWE WAFUNGUKA

WAANDISHI WETU
HUKU wakidaiwa kuogelea kwenye utajiri wa mabilioni ya fedha, nyota  wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameibukia kwenye Gazeti la Amani na kusema kuwa, amefunga ndoa ya kimyakimya na mpenzi wake wa sasa, Zarina Hassan ‘Zari’ ambaye ni nyota wa muziki wa kizazi kipya, nchini Uganda na Afrika Kusini.
Nyota  wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa na mpenzi wake Zarina Hassan ‘Zari.
Diamond aliyasema hayo juzi jijini Dar es Salaam alipofanya mahojiano na waandishi wetu baada ya kumuuliza kama ana mpango wa kufunga ndoa na Zari.
SIKIA MAHOJIANO HAYO
Amani: “Zari ameshakubebea ujauzito, ameshaandaa shoo ya nguvu ile ya Zari All White Party hapa kwenu Tanzania na ameonekana kukubalika na baadhi ya mashabiki wako. Je, una mpango gani wa kufunga naye ndoa sasa?
Diamond: “Khaa! Mbona kama ni ndoa na Zari nimeshafunga kimyakimya!”
Amani: “Si kweli bwana! Lini na wapi?”

Diamond: “Hapahapa Dar. Lakini siwezi kusema ni wapi kwani tulishaamua iwe kimyakimya na imepita tayari, siku chahe kabla ya ile shoo ya Mlimani City.”Amani: “Kama ni kweli kwa nini haikuwa na mashamsham kama ndoa za mastaa wengine?”
KISA CHA KIMYAKIMYA
Diamond: “Unajua bi mkubwa (mama yake mzazi, Sanura Kasim) alikuwa anaumwa, kidogo ana nafuu kwa sasa. Ndiyo maana sikutaka mashamsham.”Amani: “Zari mwenyewe amekubaliana na uamuzi wa ndoa ya kimyakimya?”
Diamond: “Hakuwa na shida.”

KUHUSU DINI YA ZARI
Amani: “Amebadili dini? Maana ilisemekana alikuwa Muislam, akabadili kuwa Mkristo.”
Diamond: “Ilikuwa rahisi kurudi kwenye imani yake ya kwanza kwa hiyo ataendelea kuitwa Zarina.”

DIAMOND SASA
Rafiki wa karibu wa Diamond ambaye hakupenda jina lake kutajwa gazetini lakini wengi wanamjua, alipoulizwa kuhusu ndoa ya Diamond na Zari alisema:
“Jamani! Jamani! Jamani! Hivi kweli mnavyomjua Dangote (Diamond) nyie anaweza kufunga ndoa kwa siri au kimyakimya?”


...Wakipozi.
Amani: “Amesema kwa sababu mama yake bado hajakaa sawasawa kiafya?”
Rafiki: “Mbona kaenda kutumbuiza kwenye Zari All White Party, Mlimani City, si angekaa na mama yake nyumban? Hivi Dangote mnamjua, mnamsikia? Acheni kabisa.

“Dangote anapenda kiki! Kila siku anawaza kiki. Kwa hiyo kusema amefunga ndoa na Zari sidhani kama ni kweli inaweza kuwa ni kiki. Tena afadhali kama Zari asingekuwa na mimba, lakini ameshambebea ule mzigo ndiyo kabisa maana Dangote yeye hana cha kupoteza. Lakini anyway, labda kweli.” 
NI SIKU CHACHE BAADA YA WEMA KUDAI AMEFUNGA NDOA
Hivi karibuni, mpenzi wa zamani wa Diamond aliye pia Miss Tanzania 2006 na staa wa sinema za Bongo, Wema Sepetu naye alitupia kwenye mtandao wa Instagram picha inayomwonesha amefunga ndoa kwa siri.

Baada ya picha hiyo kuwa gumzo, baadhi ya vyombo vya habari, hasa vya kielektroniki vilimpigia simu Wema ili kumuuliza kama kweli amefunga ndoa kwa siri kama inavyoenea kwenye mitandao, Wema alikiri.
Kwa ile sauti yake ndogo: “Yeah! Nimefunga kweli ndoa.”

Swali: “Sasa Wema wewe ni supastaa, kwa nini ufunge ndoa kwa siri mpaka wadau wako wasijue?”
Wema: “Mume wangu hapendi ijulikane. Hata mimi sipendi ijulikane.”

YALIYOMKUTA WEMA BAADA YA KUKIRI
Amani lilizungumza na mtu mwingine wa karibu na Wema ambapo alisema:
“Jamani Wema amejitakia matatizo, ndugu zake, dada yake na mama yake wamemjia juu. Kwanza walimuuliza kama ni kweli amefunga ndoa bila wao kujua, akasema hajafunga.

“Mama yake alimwambia alichokifanya cha kukiri kwenye redio ni nuksi kubwa kwake na Watanzania hawatamwamini tena hata akisema ukweli.“Unajua ndugu zake waliweka kikao. Walikubaliana kwamba, kama ndoa yake ilikuwa kwenye filamu si mbaya lakini walilaani kile kitendo cha kuulizwa na watangazaji wawili wa redio tena kwa muda tofauti akakiri. Pale ndipo penye tatizo. Leo hii Wema atazungumza ukweli gani kwa watu wakamuelewa?”
WEMA NA GAZETI LA AMANI
Wema alipotafutwa juzi na gazeti hili na kuulizwa kuhusu ndoa hiyo alikiri kuwa ilikuwa filamu ambayo itatoka hivi karibuni.

DIAMOND, NAY ‘WAWAVUA NGUO’ WEMA, SIWEMA!

Diamond na Nay wa Mitego wakiimba ngoma yao ya Muziki Gani.
Na Musa Mateja
DONGO! Wakali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ wameamua kuwavua nguo waliokuwa wapenzi wao kwa kuandaa wimbo ambao unazungumzia matendo machafu waliyowahi kutendewa na wapenzi wao hao.
Mashabiki wakijiachia.
Ngoma hiyo inayofahamika kama Mapenzi Pesa ambayo inaachiwa leo katika vituo mbalimbali vya redio, mastaa hao wameimba kwa staili ya kubishana kwa kuambiana kuwa mapenzi ni pesa mwingine akisema si pesa ila ni kupetipeti.
Akizungumza na Risasi Vibes, mmoja wa watu wa karibu na wasanii hao alisema kwamba, Diamond na Nay wa Mitego, wameamua kuvunja ukimya kupitia wimbo huo ambapo wamezungumza mambo yote waliyowahi kutendewa na wapenzi wao ikiwa kama njia ya kutoa kilio chao kwa jamii ambayo ilikuwa ikiwaona wao kama ndiyo wakosaji baada ya kutofautiana nao.
“Wameurekodi makusudi kabisa kufikisha ujumbe kwa mashabiki wao hasa ambao wengi hawakuweza kujua visa vya wasanii hao kuachana na wapenzi wao na kikubwa zaidi ni kuonesha kuwa mtu hata kama una pesa kiasi gani au unaonesha upendo wa aina gani lakini kama mwanamke akiamua kufanya yake, anafanya tu,” alisema mtu huyo wa karibu.


Risasi Vibes baada ya kunasa ishu hiyo, iliwasaka Diamond na Nay ili waweze kuzungumzia wimbo huo na kueleza ni kipi kilichowafanya hadi wakaamua kuingia studio na kuimba mambo ambayo kila mmoja yamemtokea kutoka kwa mpenzi wake. Majibu yao yalikuwa hivi:
“Kiukweli niliguswa sana baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wangu Siwema hasa kutokana na namna tulivyoachana, hapo ndiyo nilijua kuna baadhi ya wanawake hata uishi naye kwa mapenzi yapi na umpatie pesa kiasi gani bado suala la kutulia linategemeana na yeye tu anavyochukulia,” alisema Nay.
“Naweza kusema kuwa watu wanatakiwa kuelewa kuwa sisi ni wasanii hivyo kuna muda inatakiwa kabla hujaimba jambo kuhusu wengine basi kuna muda mzuri pia ambao tunatakiwa kuimba kuhusiana na mambo ambayo sisi wenyewe tumefanyiwa ili kuwafahamisha mashabiki wetu, najua kupitia wimbo huu kuna watakao tuelewa na wengine wataona kama tumeongea mambo ya chumbani sana lakini ukweli utabaki tu kuwa sanaa ina namna nyingi ya kufikisha ujumbe kwa mashabiki, hivyo naomba mashabiki wakae makao wa kula Jumatano (leo) watapata kila jambo ndani ya wimbo wetu huo,” Diamond.

SHABIKI WA WEMA SEPETU AFUNGUKA YA MOYONI KUHUSU MAPENZI YA WEMA NA DIAMOND PLATNUMZ YALIVYOKUWA


nanukuu kutoka kwa shabiki mtaa wa pili unajuwa watu mnaongea mengi bila ya kufikiria vizuri kama kila mtu na bahati yake.ktk mapenzi kuna mambo mengi sana alikuwa ndani ya mahusino ndio anaelewa VIZURI ninawezakana wema alijaribu sana tumia hiyo fursa lk aikwezekana jamani sio kama ameshindwa MBONA MADAME RITA ALIKUWA NA MENGI LK AKUOLEWA KWANI ALIKUWA ATAKI LK SIO BAHATI yake.tuseme jambo moja diamond ajampenda wema 100% labda 50% (ssa zari alikuwa na nguvu moja nitakupa mtoto lk fata mashariti yang) lk wema ameona kila anachojaribu kwa mwenzie akifanyia kazi ssa sio fursa wajemeni ni bahati tu.na zari kama ngekuwa mke bora mbona ameondoka kwa ivan? mke bora anavumilia kila kitu kwa mume wake kama dini zinavyosema.mara gani wema amejaribu kwa diamondo lk hakuna kitu.ok wema kashindwa peny je na jojo nae wote hakuna ata mwenye akili sio hivi kwenye mapenzi kuna siri nyingi na huyo zari ana yake kibao subiri tu

SHOO YA ZARI ALL WHITE PARTY YAFUNIKA JIJINI DAR! TAZAMA PICHA HAPA

Diamond akiwachengua mashabiki kwa wimbo wake wa Nasema Nawe aliomshirikisha Malkia wa Taarab, Khadija Kopa.
Malkia wa Taarab nchini, Khadija Kopa akiimba sambamba na Diamond Wimbo wa Nasema Nawe.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Shetta akiwarusha mashabiki waliofika katika Usiku wa Zari All White Party.
Diamond na Nay wa Mitego wakiimba ngoma yao ya Muziki Gani.
Mashabiki wakijiachia.
Diamond Platnumz akizikonga nyoyo za mashabiki.
Ray Kigosi na Mama Rolaa nao ndani.
Diamond akicheza na mashabiki wake.
Nyomi iliyohudhuria shoo hiyo.

KWA MARA YA KWANZA ZARI AFUNGUKA KWANINI ALIMKUBALI DIAMOND ALIPOMTONGOZA! SOMA HAPA


IMG_4056 
<<Mara ya kwanza ilikuwa kwenye social network tu.. nilikuwa namuonaona tu napita kwenye page yake na-like.. nilitoka kushoot video ya ‘Coco Baby’ South Africa tukakutana kwenye ndege..>>Diamond Platnumz anasimulia walivyokutana na mpenzi wake Zari kwa mara ya kwanza.

Kumbe hiki ndicho kilimvutia sana Zari kwa Diamond Platnumz>>Ni mchangamfu.. anajali.. Diamond ana akili sana, nilivutiwa nae kwa sababu ana akili sana.. anajituma sana, ni mtu mwenye malengo makubwa..>>Zari.
Kwani Diamond amewahi kuonana na watoto wa Zari?? Wanamchukuliaje? >>Bado hawajawahi kuonana.. ila watoto wanamjua.. kama mama yao nina furaha wao wana furaha pia>>—Zari.

GOOD NEWS: FAMILIA YA MAMA KIJACHO ZARI, AKIWEMO MAMA YAKE ISHAFIKA DAR KWA AJILI YA KUONANA NA DIAMOND!

Zari Earlier today with her familia at Julius Nyerere international airport, they are here to support Zari's all White Party Tonight at Mlimani City Conference Hall..#Great Love

 Zari and Sisters

Zari and Mum

Older Posts
© Copyright ZEE LA UDAKU | Designed By Code Nirvana
Back To Top