Habari Kali
Loading...

BAADA YA PICHA YA NAY NA SHAMSA FORD WAKILANA MATE KUVUJA...SIWEMA, MUME WA SHAMSA VILIO!

Mbinu Za Kumfikisha Kileleni Mwanamke Mwenye Makalio Makubwa Kwa Haraka, Bonyeza Hapa chini== >
Musa mateja na imelda mtema
Penzi matata linalowanyima usingizi baadhi ya watu mjini kwa sasa kati ya mwigizaji wa sinema za Kibongo, Shamsa Ford na mkali wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ limeibua tafrani kubwa huku waliokuwa wapenzi wa mastaa hao wakijikuta wakiangua vilio kweupe, Ijumaa limesheheni.

Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego na Shamsa Ford wakipozi kimahaba.
TATIZO MAHABA NIUE
Mara baada ya wawili hao kutangazwa rasmi kuwa sasa ni mahaba niue huku picha za ushahidi zikimwagwa, aliyekuwa mwandani wa Nay, Siwema a.k.a Wemalicious na aliyekuwa mume wa Shamsa, Dickson ‘Dick’ wanadaiwa kujikuta kwenye hali mbaya kiasi cha kumwaga machozi.

TUJIUNGE NA CHANZO KWA SIWEMA
Habari kutoka kwa chanzo chetu ambacho ni mtu wa karibu wa Siwema jijini Mwanza zilidai kwamba, mara baada ya picha za wawili hao kuzagaa kwenye mitandao ya kijamii aliumia roho hasa alipomuona Shamsa akijiachia kwenye nyumba ambayo alishirikiana na Nay kuijenga.

“Yaani Siwema ameumia hadi akajikuta akiangua kilio kwa uchungu. Sikukuu ya Pasaka ilikuwa mbaya kupita kiasi kwa Siwema. “Kinachomuuma zaidi ni kwamba hata nguo zake za mtoko Shamsa anavaa ‘gym’ na kufanyia mazoezi. Jamani kuna dharau zaidi ya hiyo? “Ukweli roho inamuuma vibaya mno,” kilisema chanzo hicho kwa ombi la kutochorwa jina gazetini.
Ney na Shamsa wakifuatilia jambo kwenye simu.
Kabla ya kuhamia kwa chanzo cha mume wa Shamsa ili kupata ubuyu kamili, gazeti hili lilimsaka Siwema ili kujua anachukuliaje jambo hilo ambapo alifunguka ya moyoni.
SIWEMA AANIKA MAZITO
Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya simu kutoka jijini Mwanza, Siwema mwenye mvuto wa kuvunja midume shingo alianika mazito kwamba, kitendo cha Nay kumuacha na muda si mrefu kwenda kwa Shamsa ni upuuzi.
Siwema alifunguka kwamba, kinachomshangaza ni kitendo cha Shamsa kuvaa nguo zake na kufanyia mazoezi.
Mwanamama huyo alisema watu watamtukana kwa kuwa hawajui tabia ya Nay kwani hata Shamsa atamshindwa tu.

“Nilivumilia vitu vingi sana. Maumivu nayajua mimi, nyumba tuliyojenga wote, anaingia mwanamke mwingine. Namhurumia sana Shamsa kwani hajui tabia za Nay,” alifunguka mtoto mweupe, Siwema kwa uchungu.
KUMBE SIWEMA ALIJUA
Habari zilieleza kwamba, Siwema alijua muda mrefu kuwa Nay anatembea na Shamsa lakini alipomuuliza staa huyo anayetamba na Ngoma ya Akadumba alimwambia walishaachana.

Siwema.
NAY ANASEMAJE?
Akizungumzia ishu hiyo, Nay alisema kuwa yeye yupo na Shamsa na kwamba anamshangaa huyo Siwema kwani alishaachana naye.

TUJIUNGE NA CHANZO KWA MUME WA SHAMSA
Kwa mujibu wa chanzo makini, naye kama Siwema, baada ya penzi la Shamsa na Nay kuwa ndiyo habari ya mjini huku wakitupia picha za malovee mtandaoni, mume wa Shamsa, Dick alipaniki kiasi cha kutokwa machozi huku akitafuta namna ya kupooza machungu.

JB AOMBWA AOKOE JAHAZI
Habari zilidai kwamba, Dick alikimbilia kwa staa wa sinema za Kibongo, Jacob Steven ‘JB’ na kwenda kumuomba aokoe jahazi akimshitakia Shamsa kuwa ameamua kumwacha na kuamua kutembea na Nay, jambo ambalo analiona kuwa ni udhalilishaji kwani ni mkewe ambaye amezaa naye mtoto mmoja wa kiume, Terry.

Mwanamuziki kinara wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Ilidaiwa kuwa, baada ya Dick kufika nyumbani kwa JB maeneo ya Ubungo-Kibangu, Dar na kumweleza hayo, mwigizaji huyo alimpigia simu Shamsa ambaye humwita Daddy na kumuuliza juu ya suala hilo ambapo alimweleza kuwa alishaachana na Dick hivyo kila mmoja ana maisha yake.
Katika hali hiyo, JB aliwataka kukaa chini na kuyamaliza kiutu uzima kuliko kuwekeana kinyongo.

SHAMSA ANASEMAJE?
Baada ya kusikia kilichopo upande wa mume wa Shamsa, gazeti hili lilimgeukia Shamsa na kumwelezea kila kitu kilichopo ambapo alionesha kumshangaa Dick kwa kuwa alishamalizana naye tangu Oktoba, mwaka jana.
“Kwanza namshangaa kwa nini anawaka wakati kila mtu ana maisha yake?“Tulishaachana tangu mwaka jana so kila mtu ana maisha yake,” alisema Shamsa ambaye kwa sasa amehamishia moyo wake kwa Nay.

Aliyekuwa mume wa Shamsa, Dickson ‘Dick’.
DIAMOND ACHAFUA HALI YA HEWA
Wakati sakata la Shamsa na Nay likishika kasi mithili ya moto wa kifuu, mwanamuziki kinara wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amechafua hali ya hewa baada ya kutundika mtandaoni picha ya mahaba ya wapenzi hao iliyosababisha tafrani zaidi.

Diamond ambaye ni swahiba wa Nay ndiye aliyekuwa wa kwanza kuweka picha iliyomuonesha Nay ‘akibusiana’ na Shamsa kupitia ukurasa wake wa Instagram hivyo kuwapandisha hasira Siwema na Dick kwani alionekana kufurahishwa na ‘pea’ hiyo.

Hizi ndio sehemu 12 zinazompa Raha mwanamke wakati wa Tendo, Bonyeza Hapa chini== >


Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA VIDEO CHAFU YA AGNESS MASOGANGE== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright ZEE LA UDAKU | Designed By Code Nirvana
Back To Top