Habari Kali
Loading...

BABA AWACHARAZA VIBOKO WALIMU WAWILI WA SHULE YA MSINGI HUKO MKOANI TABORA..

Mbinu Za Kumfikisha Kileleni Mwanamke Mwenye Makalio Makubwa Kwa Haraka, Bonyeza Hapa chini== >
Vitendo vya baadhi ya wazazi, kudhalilisha walimu vinaendelea, ambapo mzazi mmoja Selemani Juma, amewashambulia walimu wawili kwa viboko.

Amefanya hivyo kupinga mwanawe kurudishwa nyumbani, akashone kaptura. Alifanya hivyo mwishoni mwa wiki iliyopita.

Taarifa zilizomfikia mwandishi zilibainisha kuwa Juma alidhalilisha walimu wawili wa Shule ya Msingi Nzogimlole iliyopo wilayani Nzega mkoani Tabora.

Aliwashambulia kwa viboko, akipinga kitendo cha mwalimu mmojawapo, kumrudisha nyumbani mwanawe.

Mwandishi alifika katika shule hiyo, yenye walimu tisa tu na kuzungumza na Mwalimu Mkuu Msaidizi, Emmanuel Josephat, ambaye alisema mwanafunzi huyo, Shaaban Maziku anayesoma darasa la pili, alipeleka ujumbe tofauti na alioagizwa na walimu kwa baba yake, hivyo kusababisha kadhia hiyo.

Kwa mujibu wa Mwalimu Josephat, mwalimu aliyedhalilishwa (jina limehifadhiwa), alikuwa akifundisha katika darasa hilo na alipomuona mwanafunzi huyo kavaa kaptura iliyochanika vibaya, kiasi cha sehemu za siri kuonekana, alimrudisha nyumbani kwenda kurekebisha sare yake.

Mwalimu Josephat alisema mwalimu huyo wa kiume wa darasa la pili, alimwagiza mwanafunzi wake aende kwa baba yake, akamuombe amsaidie kushona kaptura hiyo.

‘’Mwalimu hana kosa, kwani mtoto kaptura  yake ilikuwa imechanika vibaya kiasi cha sehemu zake za siri kuonekana… walimu hatupaswi tuwaache hivi watoto, mwalimu alichofanya ni kumwambia akamwambie baba yake aishone ile sare, lakini mambo hayakuwa hivyo,’’ alisema Mwalimu Josephat.

Akizungumza kwa majonzi, Mwalimu Josephat alisema mtoto huyo alipofika nyumbani, alimweleza baba yake kuwa mwalimu huyo, amechana kaptura hiyo na amemwagiza arudi nyumbani kwenda kumwambia baba huyo aishone.

Ujumbe huo unadaiwa kusababisha mzazi huyo, kufika shuleni na kuanza kutoa lugha chafu dhidi ya mwalimu huyo na baadaye baba huyo alianza kutoa kipigo.

Mwalimu Josephat alidai kuwa baba huyo, alianza kutumia mawe kurusha kwa walimu hao. Baadaye alitumia fimbo, kumchapa mwalimu huyo wa darasa la pili.

Hatua hiyo inadaiwa ilisababisha mwalimu huyo, kupiga mayowe kuomba msaada. Wananafunzi waliokuwa darasani, walitoka na kuanza kumsaidia kupiga kelele za kuomba msaada.

Mayowe hayo yalisaidia mwalimu mwenzake, Elias Kafiku kutoka ofisini kwa nia ya kuamua ugomvi huo ili wazungumze kiofisi na kufikia muafaka. Lakini, mwalimu huyo pia aliambulia kipigo.

Kutokana na kipigo hicho, mwalimu huyo wa darasa la pili alipata majeraha na kupelekwa zahanati ya kijiji, ambako alipatiwa huduma na kuruhusiwa kurejea nyumbani.

Akizungumza na mwandishi, mwalimu huyo wa darasa la pili alisema hali yake inaendelea vizuri. Alisema sababu ya kupigwa na mzazi huyo, hazijui kwa kuwa alitekeleza majukumu yake kama kawaida.

 Akitoa maoni yake kuhusu tukio hilo, Mwalimu Elizabeth Kafulila wa shule hiyo, alisema tukio hilo limewatia hofu katika utendaji kazi, kutokana na mzazi kuingilia majukumu ya walimu.

Mwalimu Elizabeth aliwataka wazazi kujirekebisha na kushirikiana na walimu katika kulea watoto wao, na wanapokuwa na malalamiko, wafuate taratibu za kiofisi.

Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Suzan Kaganda alisema   mzazi huyo anashikiliwa kwa tuhuma za kupiga na kujeruhi vibaya na atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Tukio hilo limekumbushia tukio la mwaka 2009 ambapo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, Albert Mnali, aliamuru askari kucharaza bakora walimu wa shule za msingi wa wilaya hiyo.

Mnali anadaiwa aliwaamrisha askari Polisi kuwacharaza viboko walimu hao, kutokana na kusababisha wanafunzi kufeli mitihani pamoja na pia kuchelewa kazini.

Walimu walioripotiwa kuchapwa viboko na Mkuu huyo wa Wilaya ni wa shule za msingi za Katerero, Kanazi na Kasenene mkoani Kagera.

Walimu karibu nchi nzima, walilaani kitendo hicho, wakisema kimewadhalilisha na kimekiuka haki za binadamu.

Baadaye, Serikali ilichukua hatua ya kumstaafisha kazi Mkuu huyo wa Wilaya.

Hizi ndio sehemu 12 zinazompa Raha mwanamke wakati wa Tendo, Bonyeza Hapa chini== >


Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA VIDEO CHAFU YA AGNESS MASOGANGE== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright ZEE LA UDAKU | Designed By Code Nirvana
Back To Top